• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

"ANZISHENI USHIRIKA KUPATA BEI NZURI ZA MAZAO YENU"

imetumwa: July 17th, 2018

Hiyo ni kauli ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania MHE. Majaliwa Kassim Majaliwa aliyoitoa leo katika ufunguzi wa

Soko na Ghala la kuhifadhia mazao lililojengwa kwa ufadhili wa kitengo kilichopo katika Ofisi ya Waziri mkuu kijulikanacho kwa jina

la MIVARF, Soko na Ghala vimejengwa katika kata ya Bulige ambapo ni maarufu kwa ulimaji wa zao Mpunga ambapo zaidi ya asilimia ya 60 ya

Mpunga unaopatikana kanda ya ziwa huzalishwa maeneo haya. MHE. Kassim Majaliwa amewataka wananchi wa Bulige na maeneo yanayoizunguka

kuanzisha Ushirika kama wanavyofanya wananchi wa Lindi na Mtwara ili kuweza kupata bei nzuri za mazao yao kwani mazao huuzwa kwa ushindani

na hivyo kumwezesha mkulima kuuza kwa bei nzuri, MHE. Waziri Mkuu amemtaka Mkuu wa idara ya Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji kusimamia hili

kwa kuhakikisha anawaunganisha wakulima na kuwawezesha kuhifadhi mazao yao sambamba na kuwakutanisha na wanunuzi wa mazao hayo.


Suala la huduma za Afya nalo halikuachwa nyuma kwani ili kuweza kufikia Uchumi wa kati wa nchi yetu ni lazima afya za wananchi wetu ziwe nzuri

hivyo Serikali ya awamu ya tano imejiongeza bajeti ya ununuzi wa madawa na vifaa tiba na hivyo mwananchi aendapo zahanati ahakikishe anapewa dawa

na si kuonyeshwa duka la dawa lililopo karibu na zahanati. Pia MHE. Kassim Majaliwa aliwataka wanabulige kujiunga na Mfuko wa bima ya Afya ya Jamii

wanaoupenda kwani magonjwa hayana taarifa yanapokuja, yaweza kuja wakati huna pesa na hivyo ukalazimika kuuza mifugo au mazao kwa bei ya hasara hivyo

kateni bima ili ziwasaidie, amezitaja baadhi ya bima hizo kuwa ni Bima ya Afya ya Jamii (CHF iliyoboreshwa) ambapo mwananchi atatibiwa ndani ya Mkoa

wake ambapo mwananchi atachangia Tsh. 30000 kwa mwaka na atapatiwa huduma yeye na wategemezi wengine 5 mwaka mzima bure. Pia kuna bima ya ushirika

ambapo mwanachama huchangia Tsh. 76000 kwa mwaka na hutibiwa sehemu yeyote Tanzania katika Hospitali za Serikali, hii inahusisha pia matibabu katika

Hospitali za Rufaa kama KCMC, MBEYA, MUHIMBILI.


Waziri Mkuu ameahidi kutoa pesa tena ili kuongeza Ghala katika sehemu nyingine ya Halmashauri ya Msalala sambamba na kuleta gari la kubebea wagonjwa

(Ambulance), MHE. Waziri Mkuu ameupongeza uongozi wa Halmashauri kupitia Mkurugenzi mtendaji, Mwenyekiti wa Halmashauri, Wakuu wa Idara na Baraza zima

la Madiwani kwa uamuzi wa kuruhusu wafanyabiashara kufanya biashara katika eneo hilo bure kwa muda wa Miezi 6.


Nae Mbunge wa Jimbo la Msalala ameshukuru Serikali kwa kufanikisha ujenzi wa Soko na Ghala ambavyo kwa sasa vinatumika, huu ni ukombozi kwa wananchi wa

Bulige. Jambo ambalo wanabulige wanaiomba Serikali ni kuwezesha wananchi wa Bulige na jimbo la Solwa kuanzisha kilimo cha umwagiliziaji kwani maeneo haya

yana mbuga nzuri inayofaa kwa kilimo muda wote. Pia pana changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama licha ya kuwepo mradi wa maji ya ziwa Viktoria

kwani mabomba yamekuwa yakipasuka mara kwa mara na mwisho amebainisha ubovu wa barabara zinazotumika ndani na nje ya Msalala na ameomba Serikali kutatua

changamoto hizo sambamba na kuwaalika wawekezaji kuleta mashine za kukoboa Mchele kwani miundombinu yote muhimu ya uanzishaji viwanda hivyo vipo na

Halmashauri ipo tayari kutoa maeneo ya ujenzi wa viwanda hivyo bure.


Mhe. Waziri Mkuu amehitimisha ziara yake katika Halmashauri ya Msalala kwa kujibu changamoto zilizojitokeza kwa kumtaka mhandisi wa maji afuatane nae mchana

wa leo atakapoondoka kwa ndege kuelekea Dares salaam ili akanunue kifaa cha kupunguza kasi ya maji toka bomba kubwa na hivyo kuwezesha wakazi wa Bulige

kupata maji kwa uhakika. Waziri mkuu amemkaribisha naibu waziri wa ujenzi na miundombinu MHE. Kwandikwa mbunge wa Jimbo la Ushetu ambaye ameeleza jitihada

zinazofanyika kuhakikisha barabara zote zinapitika muda wote ikiwemo barabara ya Kahama Mwanangwa kuwekewa lami hapo baadae, pia NTALULA itaendelea na marekebisho

ya barabara zilizoharibika kwa mvua ili ziweze kutumika.


Na mwishoni amemkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Kahama mpya ndugu. Anamringi Macha kuwasilimia wananchi wa Bulige, ndg. Macha amemshukuru Rais kwa kumteua katika nafasi

hiyo na kuwaomba wananchi wote ndani ya Wilaya ya Kahama kutoa ushirikiano ili kuwezesha malengo yaliyowekwa na Serikali kufikiwa kwa urahisi.


Imetolewa na kitengo cha Habari na Mawasiliano Halmashauri ya Msalala.



Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.