• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA BAJETI YA 2019/20

imetumwa: January 19th, 2019


Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Msalala limepitisha bajeti ya Halmashauri ya Msalala yenye thamani ya Tsh: Bilioni 2.1 huku vipaumbele vya bajeti hiyo vikiwa vimewekwa kwenye suala la uwekezaji na ukusanyaji mapato na kuboresha vyanzo vya mapato vilivyopo sambamba na kubuni vyanzo vipya. Halmashauri katika mwaka wa fedha 2019/20 imejipanga kujenga uzio katika minada ya Bulige na Masabi ili kurahisisha zoezi la kukusanya ushuru katika minada hiyo sambamba na kujenga stendi katika kata za Segese, Isaka na Bulige.

Akiwakilisha makadirio ya bajeti ya mwaka wa fedha 2019/20 kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji , Afisa mapato bwana Samwel Seritongwe amesema Halmashauri imeamua kuandaa bajeti yenye uhalisia na hivyo kujiepusha na kuwa na bajeti isiyotekelezeka kwani kwa miaka 2 iliyopita Halmashauri iliandaa bajeti ikiwa na matarajio ya Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu ungeongeza uzalishaji suala ambalo bado mgodi huo haujaongeza uzalishaji huo mpaka sasa. Ni vizuri kuandaa bajeti kutokana na vyanzo tulivyonavyo na endapo kuna fedha itapatikana nje ya bajeti mwongozo wa bajeti unaruhusu ongezeko hilo kuingizwa kwenye bajeti kwa kufanya marekebisho ya bajeti muda wowote.

Wajumbe wa Baraza hilo wakiongozwa na mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Mibako Mabubu wameridhia makadirio hayo na kumwomba mkurugenzi Mtendaji na wataalamu wa Halmashauri kuhakikisha vyanzo vyote vya mapato vinasimamiwa kwa ufasaha sambamba na kuomba chanzo cha upimaji ardhi kwa kutumia makampuni katika kata za Segese, Mega, Bugarama, Bulyanhulu, Bulige na Isaka liingizwe ili kuongeza mapato ya Halmashauri, suala ambalo Mkurugenzi Mtendaji (W) amesema lipo kwenye bajeti na hivyo baraza likaomba mambo yote yaliyopitishwa katika bajeti hiyo yatekelezwe kwa vitendo.

Kwa upande mwingine Mkurugenzi Mtendaji (W) amesema Serikali ilizitaka Halmashauri kuwasilisha maandiko ya miradi ya jamii ili Serikali iweze kuleta fedha za kumalizia miradi viporo zilizopo kwenye maeneo yetu suala ambalo Halmashauri ililipokea na kupeleka maandiko kupitia Mbunge wa jimbo la Msalala na tayari Serikali imeyapokea maandiko hayo na muda wowote kuanzia sasa fedha za miradi ya kijamii itaingizwa na kutumwa kwa ajili ya utekelezaji hivyo Serikali itatekeleza shughuli za miradi ya kijamii kupitia maandiko yaliyowasilishwa TAMISEMI sambamba na kuwapa wadau wetu shughuli ambazo tungependa ( jamii )  itekelezwe kwani shughuli za sasa ni lazima mahitaji yatoke kwa wananchi.

IMETOLEWA NA KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO

MSALALA

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.