• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Chama Charidhiswa na maendeleo yaliyofikiwa

imetumwa: October 30th, 2023

Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga kimeridhishwa na shughuli za maendeleo zinazofanywa na Halmashauri ya Msalala kupitia wataalamu mbalimbali kutoka ngazi ya kijiji,kata na Halmashauri

kwani fedha nyingi zinazoletwa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzani Dr.Samia Hassain Suluhu,zinatendewa haki kwa kukamilisha miradi iliyokusudiwa kwa viwango

vya hali ya juu.Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kahama Mhe.Thomas myonga wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani kilichoketi 30.10.2023 kujadili taarifa za shughuli za

utekelezaji za Halmashauri kwa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023-24,mwenyekiti huyo amewapongeza Waheshimiwa Madiwani kwa kusimamia vema miradi ya maendeleo katika maeneo yao na hivyo kutekeleza ilani

ya CCM kwa vitendo. Mhe,Myonga pia amewapongeza viongozi wa vyama rafiki ndani ya Wilaya ya Kahama kwa kushirikiana na chama Tawala katika kupanga,kushauri na kukubaliana kwenye mambo ya msingi yanayohusu

maendeleo ya wanakahama,Shinyanga na Tanzania kwa ujumla kwani Rais wetu anafanya maendeleo kwa Watanzania wote na sisi kama wanasiasa tunajukumu la kuungana kwa pamoja na tufanye siasa za maendeleo kwani

mwisho wa siku tunahitaji maendeleo kwa taifa letu.


Awali akifungua kikao hicho,mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala Mhe,Mibako Mabubu ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dr.Samia Hassain Suluhu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa

kuona umuhimu wa wananchi wa Halmashauri ya Msalala kuwa na jengo lao la Utawala kwa kutoa fedha na kuwezesha jengo la Halmashauri hiyo kukamilika na kuanza kutumika,sisi kama viongozi wa Halmashauri

tunaahidi kutekeleza miradi yote iliyoletewa fedha kwa viwango vya juu na kwa wakati ili wananchi wanufaike kwa wakati na matunda ya Mhe.Rais wetu Dr.Samia Suluhu,kwa kweli haijawahi kutokea tangu ndani

ya Halmashauri kupokea fedha nyingi kiasi hiki na kufanikisha kukamilisha miradi mingi yenye mabilioni ya fedha,tunashukuru sana Rais wetu na tunakuombea kwa Mungu afya njema ili uendelee kututumikia

wananchi kwani tuna imani kubwa sana na wewe.Hoja hii imeungwa mkono Waheshimiwa Madiwani wote wa baraza hilo,baadhi ya waliounga mkono hoja hii ni Mhe,Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri na diwani wa kata

ya Mwalugulu ambaye amesema,Dr.Samia Suluhu amewezesha ongezeko la wasomi na kutoa ajira kwa kuboresha elimu,nae diwani wa Kata ya Mega Mhe.Patrick Mazuri amempongeza Mhe.Rais Samia Suluhu kwa kuwezesha

kuwezesha umeme kufika vijijini na kuchochea maendeleo kwa haraka na Mhe.Joseph Manyara diwani wa kata ya Segese ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kutoa huduma bora za afya kwani upatikanaji wa

dawa katika Halmashauri ni mzuri hivyo kuhakikisha afya za wananchi zinalindwa na akaiomba Halmashauri kumpatia greda kwa ajiri ya kuchonga barabara za Segese ambapo gharama za Mafuta wananchi wa Segese

watachangia.


Baraza limejadili kwa kina taarifa za utekelezaji za kila kata na kuomba wataalamu wazipitie kwa utulivu na kutoa majibu ya changamoto zilizowasilishwa ikiwemo utoaji wa makadirio ya majenzi yasiyoendana

na uhalisia wa bei sokoni,wananchi waliofanya kazi na Tanesco(REA) kutokulipwa fedha zao kwa wakati na kuomba wataalamu wa Halmashauri kuiga mfano wa mkurugenzi Mtendaji(W) NDG.Khamis Katimba wa kutembelea

maeneo mbalimbali ndani ya Halmashauri, hii inamsaidia kuijua vizuri Halmashauri yake hivyo wakuu wa idara fuateni nyendo za kiongozi wetu.Hoja hii imetolewa na Mhe.shija Luyombwa diwani wa kata ya Bulyanhulu

ambapo amempongeza Mkurugenzi Mtendaji(W) na wajumbe wa Baraza la Madiwani kwa usimamizi wao madhubuti wa miradi na kuwezesha Halmashauri kuhamia kwenye jengo jipya hii yote imetokana na jitihada za Mhe.Rais

Samia Suluhu kwa kutoa fedha kuwezesha miradi viporo kukamilishwa na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.Diwani huyo amemshukuru pia Mbunge wa jimbo la Msalala Mhe.Alhaji Idd Kassim Idd kwa kuisemea vizuri Halmashauri

na kushawishi Bunge kupitisha bajeti za kutekeleza miradi ndani ya Halmashauri.Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji(W) NDG.Khamis Katimba amepokea shukrani zilizotolewa na kuongeza kusema Halmashauri ipo kwa ajili

ya kuwatumikia wananchi hivyo wakati wowote yupo tayari kutumika na kuwaomba Madiwani hao kushirikishana uzoefu wa changamoto wanazokutana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku kwa kuwa changamoto

hutofautiana kulingana na mazingira yao ya kiutawala,Halmashauri ndani ya mwezi ujao itaanza maandalizi ya mpango na bajeti kwa mwaka ujao hivyo vipaumbele vya kila kata vitazingatiwa kwakuwa tayari mwongozo

upo kupitia sensa ya watu na makazi iliyofanyika 2022.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.