• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Kamati ya fedha, uongozi na mipango yataka miradi ikamilishwe kwa wakati

imetumwa: September 2nd, 2019

Kamati ya fedha, uongozi na mipango ya Halmashauri imewataka wamiliki wa mashamba yanayochimbwa madini na wamiliki wa migodi ya wachimbaji wadogo wadogo kuhakikisha makubaliano waliyowekeana na Halmashauri yanatekelezwa na kukamilika kwa wakati ili miradi hiyo ianze kutumika na jamii. Miongoni ya miradi hiyo ni ujenzi wa zahanati katika kitongoji cha kakola namba 9 ili kuwezesha jamii ya maeneo hayo kufaidika kutokana na uwepo wa uchimbaji madini.

Agizo hilo limetolewa leo wakati wa kikao cha kamati hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo ambapo mwenyekiti wa kikao hicho MHE. Mibako mabubu amewataka wataalamu kusimamia maelekezo yaliyotolewa na kamati hiyo. Katika kikao hicho wajumbe mbalimbali wamehudhulia akiwepo mbunge wa jimbo la Msalala MHE. Ezekiel Maige, mwakilishi wa katibu Tawala (M) bwana Kasani, wajumbe wa kamati hiyo na wataalamu wa Halmashauri.

Masuala mengine yaliyojadiliwa katika kikao hicho ni Halmashauri kuhakikisha mapato yanayokusanywa yanapelekwa benki kwa wakati ili kujiepusha na hoja za ukaguzi ambapo kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo ndugu Masatu Mnyoro amesema tayari kamati tendaji imeanza kuchukua hatua stahiki kwa wakusanya mapato ambao bado hawajapeleka fedha benki sambamba na hilo wajumbe walitaka watumishi kuwatumikia wananchi kwa moyo mmoja na kujiepusha na kuwanyanyasa wananchi kwani jamii inawategemea sana wataalamu hao.

Nae MHE. Frola Sagasaga diwani wa kata ya Mwalugulu ametaka Halmashauri kuchukua tahadhali kwa kuhakikisha inasimamia ujenzi wa vyoo na uhifadhi wa mazingira katika maeneo yote yanayojihusisha na uchimbaji dhahabu na hasa katika eneo la namba 9 na namba 2 kwani maeneo hayo hali ya usafi hairidhishi na isitoshe tunaelekea katika msimu wa mvua za masika hivyo hali hiyo ikiachwa iendelee ni dhahili kuwa ugonjwa wa kipindupindu unaweza kutokea na hivyo kuathiri afya za wananchi, suala ambalo limeungwa mkono na wajumbe wote wa kamati hiyo. Akijibu hoja hiyo ndugu Masatu Mnyoro amesema suala hilo lipo katika utekelezaji kwa kuwa tayari mkuu wa Wilaya alishatoa maelekezo na hata hivyo Halmashauri inalichukua kwa utekelezaji.

Akihitimisha kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo amewataka wajumbe wa kamati hiyo kufanya kazi kwa umoja kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanaletewa maendeleo hasa katika kuhakikisha mapato yanakusanywa kwani kila diwani ana wajibu wa kuhakikisha katika kata yake vyanzo vilivyopo anavisimamia na  kutoa taarifa Halmashauri ili kuwezesha Halmashauri kujipatia mapato. Ameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kuanzisha soko la dhahabu katika eneo la uzalishaji kwani imekuwa ni chanzo kizuri cha mapato kwa Halmashauri.

Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Halmashauri ya Msalala

  

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.