• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Sherehe Mei Mosi zatia Fora

imetumwa: May 1st, 2024

Sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani nchini Tanzania zimeadhimishwa kitaifa mkoani Kilimanjaro huku Mkoani Shinyanga zikiadhimishwa kimkoa katika kijiji cha Kakola kata ya Bulyanhulu

Halmashauri ya Msalala Wilayani Kahama ambapo mkuu wa Mkoa wa Shinyanga MHE.Anamringi Macha amekuwa mgeni Rasmi katika Sherehe hizo.Taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi zimeshiriki maadhimisho hayo

huku Kauli mbiu ya Mei Mosi ya mwaka 2024 ikiwa ni  nyongeza ya Mishahara ni msingi Bora na kinga ya hali Ngumu ya Maisha.


MHE.Anamringi Macha amewataka Watumishi kuendelea kuchapa kazi kwa bidii na ari kubwa ili kuhakikisha tunainua vipato vya mtu binafsi,mkoa na Taifa kwa ujumla kwani kupitia jitihada za mwananchi mmoja mmoja

ndipo maendeleo ya nchi yetu yanaweza kufikiwa kwa urahisi na akatoa wito kwa wafanyakazi wanaofanya kazi kwa mazoea kuacha tabia hiyo kwani ni kukwamisha jitihada na malengo ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa

na MHE.Rais Samia Suluhu anayehitaji wananchi kuwezeshwa kiuchumi ili kuinua pato la nchi na ni wafanyakazi wa Tanzania tunategemewa kufanikisha hili hivyo tujitoe kwa moyo wote kuwatumikia wananchi wetu.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kahama MHE.Mboni Mhita ameyapongeza mashirika mbalimbali ya Umma na Binafsi,Halmashauri za Wilaya,Manispaa,Ofisi za wakuu wa Wilaya za mkoa wa Shinyanga, Wanahabari na wananchi wote walio

jitokeza kwenye sherehe za maadhimisho ya sikukuu za Wafanyakazi kwani sherehe hizi ni zetu,nimefurahi kuona umati mkubwa wa Watumishi na wananchi kutuunga mkono yote hii ni kukubaliana na mazuri yanayofanywa na Serikali yetu

ya awamu ya sita,sio siri yanayofanywa na MHE.Rais Samia Suluhu yanaonekana,naomba miradi yote iliyokamilika ndani ya Halmashauri tuitunze kwa kuwa ni mali yetu.


Nae MHE.Mbunge wa Jimbo la Msalala MHE.Alhaji Idd Kassimu Idd licha ya Vikao vya Bunge kuendelea amehudhuria Sherehe hizi na kuweka bayana Baadhi ya Miradi iliyotekelezwa na kukamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi kuwa

ni Shule ya Msingi Bulyanhulu,Shule ya Sekondari Bushingwe,Kituo cha Afya Bugarama,Shule ya Sekondari ya Wasichana Bulyanhulu.Hii ni baadhi ya Miradi iliyotekelezwa na Serikali yetu inayoongozwa na MHE.Rais Samia Hasain Suluhu

kwa kweli Kwa niaba ya wananchi wa Halmashauri ya Msalala tunamshukuru sana kwa kutuletea mabilioni ya fedha kukamilisha miradi mingi ya maendeleo ndani ya Halmashauri ya Msalala,haijawahi kutokea kupokea fedha nyingi ndani ya

mda mfupi.Mda si mrefu barabara yetu ya Kakola Kahama nayo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami hivyo Wafanyakazi tuone fahari kuwatumikia wananchi kwani MHE.Rais anahitaji wananchi tuwatumikie kwa ufasaha.


Nae Mwakilishi wa TUCTA Mkoa NDG.Ramadhani Pangara ametaja baadhi ya changamoto zinazowakabili Wafanyakazi Mkoani Shinyanga kuwa ni kuchelewa kulipwa mafao kwa Wastaafu,Kikokotoo kiangaliwe kwa upya kwani kinatuumiza Wafanyakazi, baadhi ya Waajiri

kutopeleka michango ya Wafanyakazi wao kwenye Mifuko ya hifadhi ya Jamii na kuomba Serikali kuyapatia ufumbuzi changamoto hizo. Akihutubia Wafanyakazi Mkuu wa Mkoa huyo ameahidi kuzipatia ufumbuzi mapema changamoto zilizowasilishwa kwani Serikali

yetu ni sikivu hasa katika suala la kikokotoo mana changamoto hii ni ya nchi nzima hivyo suluhisho litapatikana kwa bahati nzuri pia Wabunge wetu wameishaishauri Serikali kupitia vikao vya Bunge letu hivyo Wafanyakazi wenzangu tuwe na uvumilivu wakati

Serikali ikiendelea kulifanyia kazi.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.