• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji nyuki
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Aridhi na Nyumba

Idara ya Ardhi, Maliasili na Mazingira

Halmashauri ya Msalala ina ukubwa wa Km2 2,635.2 ambazo ni sawa na asilimia 5.2 (%) ya eneo lote la Mkoa wa Shinyanga. Jumla ya kaya 39,999 zenye watu 250,727 (Ke 128,498 na me 122,234) Sensa ya watu na Makazi Mwaka 2012), hivyo kufanya msongamano wa watu katika eneo la makazi kufikia watu 93.4 kwa Kilometa mraba 1.

Halmashauri ya Wilaya ya Msalala inapatikana kati ya Latitude 3015’’ na 4030’’ kusini mwa Ikweta na Longitude 31030’’ na 330000’’ Mashariki mwa Greenwich. Kaskazini inapakana na Mkoa wa Geita, Kusini inapakana na Mkoa wa Tabora, Mashariki inapakana na Wilaya ya Shinyanga na Magharibi inapakana na Halmashauri ya Mji wa Kahama.

Ramani 1.Ramani ya Mkoa wa Shinyanga kuonesha Halmashauri ya Msalala

Ramani 2. Ramani ya Wilaya ya Kahama kuonesha Halmashauri ya  Msalala

  •  
  • Kitengo cha Mipango Miji
  • Mafanikio
  • Uandaaji wa michoro ya Mipango Miji.

Katika kutekeleza majukumu yake,Idara imefanikiwa kuandaa michoro ya Makao Makuu ya Halmashauri ya Msalala katika Kata ya Ntobo pamoja kutangaza maeneo ya Ntobo, Masabi na Segese kuwa maeneo ya Mpango Mji (Planning Area).

Jumla ya michoro (5) ya mipango mji katika eneo la makao makuu Ntobo na Masabi imeandaliwa na tayari imeshapitishwa na kuidhinishwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Pia tumehuisha mchoro 1 na kuandaa mwingine 1 katika eneo la Itogwanholo, Kata ya Isaka. Michoro yote 7 ina jumla ya viwanja vya matumizi mbalimbali 4,175. Aidha Michoro yote hii imekwisha idhinishwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.(Rejea ramani 1,2,3)

Ramani 3. Ramani ya mchoro wa mipango miji eneo la Ntobo Makao Makuu.


Ramani 4.Ramani ya mchoro wa Kutangaza maeneo ya Mipango Miji.

Jedwali 3. Muhtasari wa Michoro na Idadi ya Viwanja (Makao Makuu)

NA
JINA LA MCHORO
TP  NO (NAMBA YA MCHORO)
IDADI YA VIWANJA
1
Ntobo central area layout plan
TP DRG No 16/MDC/15/052016
575
2
Masabi neighbourhood layout I
TP DRG No 16/MDC/19/082016
737
3
Masabi neighbourhood layout II
TP DRG No 16/MDC/20/082016
823
4
Ntobo neighbouhood layout I
TP DRG No 16/MDC/16/072016
621
5
Ntobo neighbouhood layout II
TP DRG No 16/MDC/17/072016
435

Jumla

3191

Jedwali 4.Muhtasari wa Michoro na Idadi ya Viwanja(Maeneo mengine)

NA
JINA LA MCHORO
TP  NO (NAMBA YA MCHORO)
IDADI YA VIWANJA
1
Itogwanholo squatter upgrading layout plan IV
TP DRG No 16/MDC/14/042016
687
2
Itogwanholo neighbourhood unit V
TP DRG No 16/MDC/18/082016
297

JUMLA

984

Jedwali 5. Uandaaji michoro midogo ya kina (Site-plan)

NA
JINA LA KATA
SHUGHULI
MATOKEO
1
KATA YA BULYANHULU
Kuandaa mchoro mdogo wa kina wa eneo la ujenzi wa Shule ya Msingi Kabale
Mchoro umekamilika na Ujenzi wa Shule hiyo umekamilika.
2
KATA YA ISAKA
Kuandaa mchoro mdogo wa kina wa eneo la ujenzi wa kituo cha Afya
Mchoro umekamilika na tayari ujenzi umeanza
3
KATA YA MWAKATA
Kuandaa mchoro mdogo wa kina wa eneo la ujenzi wa Sekondari ya Kata ya Mwakata
Mchoro umekamilika na tayari ujenzi umeanza
4
KATA YA IKINDA
Kuandaa mchoro mdogo wa kina wa eneo la ujenzi wa shule ya MsingiBuzima na Nyakadoni
Michoro imekamilika, na imekabidhiwa serikali ya kijiji tayari kwa ujenzi.
5
KATA YA LUNGUYA
Kuandaa mchoro mdogo wa kina wa eneo la ujenzi wa shule ya Msingi Nyangalata
Mchoro umekamilika, mchoro umekabidhiwa serikali ya kijiji tayari kwa ujenzi.
6
KATA YA MEGA
Kuandaa mchoro mdogo wa kina wa eneo la ujenzi wa shule ya Sekondari Mega
Mchoro umekamilika, mchoro umekabidhiwa viongozi wa kata tayari kwa ujenzi
  •  Kitengo cha Upimaji
  • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala imerithi jumla ya viwanja vilivyopimwa 1,978 kutoka Halmashauri ya Kahama,kati ya viwanja hivyo jumla ya viwanja 1,962 vimeidhinishwa na viwanja 16 ni vya upimaji wa awali (dermacation).

Jedwali 6.Takwimu za viwanja vya zamani

NA
Sehemu Kilipo

Viwanja vilivyoidhinishwa

Viwanja Hatua ya Demarcation

Jumla
1
Isaka
582                  
-
582
2
Bugarama
336
-
336
3
Ilogi
627
-
627
4
Segese
85
15
100
5
Ntobo
331
00
331
6
Kakola
1
1
2
Jumla
1962
16
1978

Aidha katika kipindi cha mwaka 2016-2017 Idara imefanikiwa kupima jumla ya viwanja 414 Mchanganuo wa viwanja hivyo ni kama ifuatavyo hapa chini.

Jedwali 7.Takwimu za viwanja vipya (2016-2017)

NA
SEHEMU KILIPO
NAMBA YA USAJILI MCHORO
IDADI YA VIWANJA
1
Isaka
Plan No E21 84/35     Reg.88808
07


Plan No E21 84/36     Reg.88809
07


Plan No E21 84/37     Reg.88810
08
2
Segese
Plan No E21 196/31   Reg.88658
28


Plan No E21 196/32   Reg.88659
32
3
Ntobo
Plan No E21 196/36    Reg.20130
45


Plan No E21 196/35    Reg.20129
67


Plan No E21 196/33    Reg.88830
131


Plan No E21 196/34    Reg.88831
89
JUMLA KUU
414

Kitengo cha Usimamizi wa Ardhi. 

Kitengo cha Ardhi katika Usimamizi wa Ardhi kwa mwaka 2016/2017 imefanikiwa kutekeleza majukumu yake kama ifuatavyo:

  • Utoaji wa Hati

Jumla ya hati 123 zimetolewa, kwa mwaka 2016 imetoa hati 81 na kwa mwaka 2017 imetoa hati 42, pia hatimiliki 5 za kimila zimetolewa.

  • Ukusanyaji wa  kodi

Jumla ya Tshs 67,043,058.23 zimekusanywa.Kwa mwaka 2016 imekusanya Tshs 22,347,686.08 na kwa mwaka 2017 imekusanya Tshs 44,695,372.15

  • Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi

Migogoro ya Ardhi iliyosikilizwa na kutatuliwa kipindi cha mwaka 2016/2017 ni kama ilivyo ainishwa kwenye jedwali hapa chini.

Jedwali 8.Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi maeneo mbalimbali

JINA LA MGOGORO

AINA YA MGOGORO

ULIVYOENDESHWA

ULIVYOISHIA

AGUSTINO MAFWELE NA SERIKALI YA KIJIJI CHA ISAKA STATION
Mgogoro wa eneo
  • Lalamiko hili ni la muda mrefu sana tangu 2003
  • Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala alifika na wataalamu kutoka Idara ya Ardhi na kukaa kikao na wanakijiji
  • Eneo hilo lilikuwa ni soko kwa mujibu wa upimaji 2003.
  • Wakatiwakubadilimatumiziyaeneohiliwotewaliokuwanauwezowakuendelezamaeneoyaokwakujenganyumbazakudumuwaliruhusiwakuyaendeleza
  • Mmilikiwaawaliwaeneohilialikuwananyumbayamitinakwawakatihuohakuwanauwezowakuliendelezaeneohilo.
  • Alipewa eneo mbadala la ekari moja sehemu ya barabara ya sita ambalo mpaka leo anaendelea kulimiliki.
  • Kwa kuwa mji mdogo wa Isaka ulitangazwa kuwa eneo la mpango miji kwa tangazo la serikali 1994 kwa mujibu wa sheria ya mipango miji na vijiji sura 355 na sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kifungu na 13 na kwa kuangalia ushahidi wa pande zote mbili, eneo hili lilitengwa kuwa soko kwa manufaa ya jamii ya watu wa Isaka. Mkurugenzi Mtendaji alisema Mzee Agustine Mafwele hana haki ya eneo analolalamikia
MONYIWA NA KANISA LA MOROVIAN
Mgogoro waeneo
  • Lalamiko hili ni la muda mrefu sana tangu 2003
  • Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala alifika na wataalamu kutoka Idara ya Ardhi na kukaa kikao na wanakijiji
  • Kanisa limejengwa hapo kuanzia mwaka 1991
  • Eneo hilo lilipimwa na Ndugu Monyiwa aligawiwa viwanja vipatavyo 10 ambavyo alilipwa fidia na watu wanavitumia sasa
  • Mgogoro huu ulishashuluhishwa na Halmashauri ya Kahama kabla ya kugawanyika
  • Tume ya Mkuu wa Wilaya na tume ya Naibu waziri wa Ardhi (2003)  iliyofuatilia kusuluhisha, ilitoa maamuzi kuwa eneo hilo ni halali kwa kanisa la Morovian
  • Kwa kuangalia ushahidi wa pande zote mbili, Mkurugenzi Mtendaji aliomba nyaraka za pande zote mbili ziwasilishwe
  • Pia aliomba timu ya wataalamu wafike kwenye eneo la mgogoro
Mgogoro kati ya shule ya msingi chela na lambo la kijiji
Mgogorowamipaka
  • Wataalamu kutoka ardhi walifika na kukutana na pande mbili kati ya uongozi wa shule na serikali ya kijiji.
  • Mgogoro umetatuliwa
Mgogoro kati ya shule ya sekondari Bulige na wananchi
Mgogorowaeneo
Pande zote mbili zilikutana, kati ya uongozi wa shule na wananchi pamoja na wataalamu kutoka ofisi ya ardhi
  • Mgogoro umetatuliwa.
Mgogoro kati ya zahanati ya segese na wananchi
Mgogorowa mipaka
Pande zote mbili zilikutana, kati ya uongozi wa zahanati ya segese, serikali ya kijiji na wananchi
Mgogoro umetatuliwa

Kitengo cha Uthamini

Kitengo cha Uthamini ni miongoni mwa vitengo vinavyounda Idara ya Ardhi na Maliasili,kitengo hiki kinashughulika na shughuli zote zinazohusiana na mambo ya uthamini. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017, kitengo cha uthamini kimetekeleza mambo yafuatayo:-

  • Kufanya Uthamini wa Mali za Serikali zilizopo katika Halmashauri ya  Wilaya ya Msalala. Kitengo kimefanikiwa kufanya uthamini wa mali zote za Halmashauri ikiwemo majengo, ardhi, madaraja, barabara, pamoja na vifaa vya ofisi. Katika zoezi hili jumla ya vijiji 92 vya Halmashauri vilitembelewa na mali zilizopo kufanyiwa Uthamini.
  • Utatuzi wa migogoro yote inayohusu fidia, kwa kiasi kikubwa kwa maeneo yaliyotwaliwa na halmashauri ambapo wamiliki wa maeneo wamekuwa wakidai fidia, kitengo cha uthamini kimekuwa kikishughulikia kero hizo na kuhakikisha wahusika wanapata stahiki zao.
  • Kitengo cha Uthamini kimeandaa mpango mkakati wa kuanza kukusanya kodi za majengo, kodi hizi tunategemea kuanza kukusanya mwaka wa fedha 2017/2018 ambapo mapato ya Halmashauri yataongezeka mara dufu.

Kitengo cha Maliasili

Kitengo cha maliasili kinaundwa na vitengo vidogo3 ambavyo ni kitengo cha Misitu,Nyuki na Wanyamapori.

Kitengo cha Misitu

Mafanikio

Zoezi la upandaji miti

Halmashauri inaendelea na utekelezaji wa zoezi la upandaji miti katika mwaka 2016/2017 zoezi la upandaji miti lizinduliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mh.Fadhili Nkulu tarehe 01/03/2017 akiongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala pamoja na watumishi kutoka idara mbalimbali, jumla ya miche ya miti 3,500 ilipandwa katika eneo la Makao Makuu ya Halmashauri yaliyopo Kata ya Ntobo .ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi, Halmashauri imetekeleza shughuli za upandaji miti katika kipindi cha mvua za vuli na masika katika  taasisi za Serikali ikiwa ni pamoja na  Shule za Msingi na Sekondari.

Mafanikio

  • Wakati wa msimu wa mvua za vuli na masika  (2016/2017) jumla  ya miti 24,385 imepandwa katika maeneo ya Shule za Msingi, Sekondari ofisi za Serikali pamoja na Zahanati, Halmashauri kwa kushirikiana na kikundi cha Segese Agroforestry pamoja na Ndg. Nicholous Paul mdau wa mazingira kutoka Kata ya Shilela.
  • Jumla ya miti 90,282 imepandwa kwenye kaya pamoja na watu binafsi hivyo kufanya jumla ya miti iliyopandwa 2016/2017 kuwa 114,667.

Kielelezo 59.Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mh.Fadhili Nkulu na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala Ndg, Simon Berege wakishiriki zoezi la upandaji miti lililofanyika katika eneo zitakapojengwa Ofisi za Halmashauri ya Msalala

  • Kitengo cha Nyuki

Ufugaji nyuki ni moja ya shughuli zinazofanywa na wananchi wa Halmashauri ya Msalala ili kujiongezea kipato.Jumla ya mizinga ya kisasa 595 na mizinga ya kienyeji 1,648 imetundikwa katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri.Uhifadhi wa mazingira ni moja kati ya faida kubwa zinazotokana na ufugaji nyuki katika maeneo ya misitu ilipotundikwa mizinga. Shughuli ya ufugaji nyuki inakabiliwa na changamoto ya uharibifu wa mazingira kutokana na shughuili za kibinadamu za uchomaji mkaa, kunipamoja na ukataji miti kwa ajili ya matimba yanayotumika kwenye migodi, ukosefu wa elimu ya ufugaji wa nyuki kitaalamu kwa kutumia mizinga ya kisasa (morden bee hive).

  •  
  • Kitengo cha Wanyamapori

Kitengo cha wanyamapori kimeundwa na vitengo vidogo 3 Misitu, Nyuki na Wanyamapori.

Mafanikio 

  • Ukusunyaji ushuru wa gobole na uhakiki wa silaha kila Kata ndani ya Halmashauri ya Msalala

Kitengo kimeweza kuwahamasisha wamiliki wa gobore kwa kuwaandikia barua kwa kushirikiana na Maafisa Watendaji Kata zote ndani ya Halmashauri yetu kulipia ushuru wa silaha wanazomiliki kwa wakati ili kuepuka usumbufu, sambamba na hilo pia kitengo kimefanikiwa katika utoaji wa elimu juu ya taratibu za kufuata katika umiliki wa nyara za serikali zaidi elimu hiyo ililenga waganga wajadi wanaopatikana katika kata zote ndani ya halmashauri.

  • Kuzuia vifo vya watu na mifugo na uharibifu wa mazao unaosababishwa na wanyamapori.

Kitengo kimefanikiiwa kudhibiti wanyama waharibifu zaidi ikiwa ni fisi katika kila kata walipokuwa wakijitokeza na kuvamia hivyo kusababisha vifo vya mifugo na kuhatarisha usalama wa watu waishio ndani ya kata ya hizo. Zoezi Hilo lilifanyika kwa ufanisi mkubwa kwa kushirikiana na wanakijiji wa kata husika na viongozi wao. Miongoni mwa mafanikio yaliopatikana katika shughuli hiyo ya kudhibiti wanyama waharibifu ni kama ifuatavyo:-

Ngaya ni Kata inayozungukwa na mawe makubwa ambayo inapelekea kuwa mazalia ya fisi, hivyo kutokana na uhaba wa chakula kwa wanyama hao hatarishi hupelekea kuwinda mifugo ya wakazi wa eneo hilo walioko pembezoni mwa milima hiyo na kuharibu mazao yao kama matikiti.

Katika zoezi lililofanyika siku 4 kuanzia tarehe 06/09/2016 mpaka 09/09/2016, majira ya usiku ikijumuisha Afisa Wanyamapori Msalala na Maafisa Wanyamapori wengine 2 kutoka pori la akiba la Moyowosi/Kigosi pamoja na vijana 2 (wasaidizi). Tulifanikiwa kuzunguka milima 3 kwa kutega mitego pamoja na doria za kuzunguka milima hiyo,katika zoezi hilo tulifanikiwa kuua fisi sita (6) ambao walikuwa wanahatarisha maisha ya wakazi wa eneo husika na mali zao, kwa kufuata sheria ya wanyamapori No.5 ya mwaka 2009. Pia kuna viashiria vya fisi kuwepo kwa vile bado kuna mapango ambayo ndio hasa makazi yao, hivyo baada ya zoezi hili tuliwaelekeza wananchi pindi inapotokea taarifa ya kuonekana kwa wanyama hao ifikishwe haraka ofisini kwa ajili ya kuchukuliwa hatua.

Sehemu nyingine ni Kata ya Bulyanhulu ambapo palitokea taarifa ya kuonekana fisi “spotted hyena Crocuta crocuta” ndani ya mgodi wa Bulyanhulu aliekuwa anahatarisha usalama wa wafanyakazi wa mgodi na pia kufanya shughuli za uzalishaji kusimama kwa muda. Mkuu wa Wilaya aliagiza suala hilo kushughulikiwa, hivyo kwa kushirikiana na askari wanyamapori 2 kutoka pori la Kigosi/Moyowosi mnamo tarehe 2/11/2016 mpaka 3/11/2016 aliwindwa mnyama huyo na kufanikiwa kumua majira ya saa 8 usiku na kufuata taratibu zote za sheria ya wanyamapori No.5 ya 2009 kwa ajili ya kumuhifadhi.Hivyo kuruhusu shughuli za uzalishaji kuendelea kama awali.

Kielelezo 60.Fisi alieuwawa baada ya kuvamia katika mgodi wa Bulyanhulu. 

Kielelezo 61.Wanyama hatari waliopatikana wamekufa katika Kijiji cha Kakola no.9

Kata ya Chela ni miongoni mwa kata inayozungukwa na safu za mlima wa lyandilabaloha ambapo inaaminika kuwa na wanyama hatari kama fisi na mbweha wanaoweza kushambulia mifugo na watu. Hivyo kitengo cha wanyamapori kiliunda kikosi kazi kwa ajili ya kudhibiti wanyama hao hatari mnamo tarehe 28/4/2017 mpaka 30/4/2017 kuzunguka maeneo ya Chela na kufanikiwa kuua fisi (5) na mbweha (1). Hivyo kwa idadi hiyo ya wanyama hao hatari kufa kulisaidia kupunguza uvamizi kwa mifugo ya wakazi wa maeneo hayo.

Kielelezo 62 Wanyama hatarishi waliopatakana wamekufa Kata ya Chela

 

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Tangazo la Ufadhili wa masomo toka kwa Mbunge wa jimbo la msalala October 19, 2022
  • KUITWA KWENYE USAILI TAREHE 28.02.2023 February 23, 2023
  • Pakua hapa maelekezo ya namna kujikinga na ugonjwa wa Ebola October 12, 2022
  • Sikukuu za Nane Nane July 24, 2019
  • Tazama yote

Habari mpya

  • "Nimelizishwa na kazi mnazozifanya Halmashauri"

    February 07, 2023
  • Serikali Yapania Kuondosha Utegemezi

    December 19, 2022
  • Baraza lapongeza ripoti ya ufungaji hesabu zake

    September 28, 2022
  • UN Women yaendelea kumwaga miradi Msalala

    January 25, 2022
  • Tazama yote

Video

AFSA MANUNUZI WA WILAYA PAMOJA NA LOCAL FUNDI WAMEOMBA ZABUNI PAMOJA NA UJENZI WA ZAHANATI YA NGAYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.