• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji nyuki
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Maji

TAARIFA FUPI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA IDARA YA MAJI  

 

Idara ya maji ni mojawapo ya Idara sita (6) za  Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Mkoa wa Shinyanga, Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ina Jumla ya wananchi 250,727 kulingana na Sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2012, kati ya Wananchi hao watu 129,376 wanapata huduma ya Maji  ambao ni sawa na asilimia 51.6 wanaopata maji safi na salama. Miradi ya maji ya bomba na Visima  ipo  347 inayotoa huduma ya maji katika vijiji mbalimbali vya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala  kati ya miradi hiyo visima virefu vipo 48 vilivyofungwa pampu za mkono, visima vifupi vipo 275 vilivyofungwa pampu za mkono, mabwawa 6, miradi 6 ya maji ya Mserereko(Gravity scheme) na miradi miwili inatumia nguvu ya jua Kwa sasa kuna Jumuiya za  watumia maji 21, ambapo kati ya hizo 16 zimesajiliwa na 5 zimehamasishwa ziko kwenye mpango wa kusajiliwa.

Halmashauri inategemea kuongeza huduma ya maji safi na salama kutoka 51.6 mpaka 57.08 kupitia miradi ya maji miwili inayokaribia kuanza kujengwa katika vijiji sita vya kata ya Bulyanhulu kupitia mradi wa Ushirikiano kati ya Halmashauri za Wilaya ya Msalala, Nyangh’wale na Shinyanga pamoja na mradi wa maji wa Kagongwa – Isaka ambayo ujenzi wake unategemea kujengwa kuanzia mwezi Januari na mradi wa maji wa Igombe na Mhama uliopo  kwenye hatua za mwisho za Ujenzi.

Idara ina watumishi saba (7) kwa ujumla wake ikiongozwa na Mkuu wa Idara na Mafundi Sanifu Sita (06).

Maji ni muhimu kwa viumbe vyote duniani, bila maji hakuna uhai. Aidha maji ni muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.  Kiwango cha maendeleo ya jamii yoyote kinategemea kuwepo kwa maji ya kutosha na yenye ubora unaotakiwa. Katika hali yake ya asili, maji ni sehemu ya mazingira ambapo wingi na ubora wake ndio unaosaidia katika kuamua jinsi maji yatakavyotumika.  Upatikanaji wa maji safi na salama kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na usafi wa mazingira ni muhimu katika kulinda afya za wananchi.  Utumiaji wa maji ambayo sio salama na uhaba wa maji huchangia katika kusababisha milipuko na kuenea kwa magonjwa kama kuhara na kipindupindu.  Japokuwa maji ni muhimu kwa uhai wa viumbe, na maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hakuna uwiano wa mgawanyo wa maji ulio sawa kati ya sehemu moja na nyingine na katika majira mbalimbali ya mwaka.  Aidha, wingi wa maji yanayofaa kwa matumizi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi una kikomo, na maji hayo pia yanaweza kuathirika kirahisi. 

Lengo kubwa la Halmashauri ni kuhakikisha kuwa inatoa huduma bora za maji ili kufikia dira ya maendeleo ya Taifa ya 2025 kuhakikisha kuwa 85% ya Wananchi wote wanaoishi vijijini wanapata huduma ya maji kwa umbali usiozidi mita 400.

Katika utaratibu Halmashauri iliojiwekea inategemea kuanza ujenzi wa mradi Mkubwa wa maji unaotegemea kujengwa kwa ushirikiano na Halmashauri tatu ambazo ni Msalala kama msimamizi mkubwa wa mradi, Halmashauri ya Wilaya ya Nyangh’wale,Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Vijijini na Mgodi wa madini ya Dhahabu  wa ACACIA (Bulyanhulu). Mradi huu unategewa kuhudumia vijiji 15 ambapo watu 100,437 watanufaika na huduma ya maji kwa awamu ya pili ya Ujenzi wa mradi huo.

 

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Tangazo la Ufadhili wa masomo toka kwa Mbunge wa jimbo la msalala October 19, 2022
  • KUITWA KWENYE USAILI TAREHE 28.02.2023 February 23, 2023
  • Pakua hapa maelekezo ya namna kujikinga na ugonjwa wa Ebola October 12, 2022
  • Sikukuu za Nane Nane July 24, 2019
  • Tazama yote

Habari mpya

  • "Nimelizishwa na kazi mnazozifanya Halmashauri"

    February 07, 2023
  • Serikali Yapania Kuondosha Utegemezi

    December 19, 2022
  • Baraza lapongeza ripoti ya ufungaji hesabu zake

    September 28, 2022
  • UN Women yaendelea kumwaga miradi Msalala

    January 25, 2022
  • Tazama yote

Video

AFSA MANUNUZI WA WILAYA PAMOJA NA LOCAL FUNDI WAMEOMBA ZABUNI PAMOJA NA UJENZI WA ZAHANATI YA NGAYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.