• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Tasaf

TAARIFA YA SHUGHULI ZA MFUKO WA MAENDELEO YA JAMII TASAF III, MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA 

1.0.  Utangulizi:

Halmashuri ya Wilaya ya Msalala ni moja kati ya Halmashauri zinazotekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (PSSN) chini ya TASAF III. Mpango huu ulizinduliwa rasmi hapa nchini mwaka 2012 na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani awamu ya nne Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, hata hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ilizindua rasmi Mpango huu wa Kunusuru Kaya Masikini tarehe 8 mwezi wa Octoba  mwaka 2014.

2.0. Utambuzi wa kaya Masikini

Baada ya uzindunzi  wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini zoezi la kutambua kaya masikini lilifanyika katika vijiji 64 vya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kati ya vijiji 92 vinavyofanya Halmashauri ya Msalala.  Vijiji  lengwa katika Mpango huu ni matokeo ya utafiti   uliofanywa na Kitengo cha Takwimu cha Taifa Mwaka 2002 wakati kikiendesha zoezi la kutathimini hali ya umasikini nchini. Zoezi la kuzitambua kaya masikini lilifanywa na wawezeshaji ngazi ya Wilaya kwa kushirikiana na Serikali za Vijiji husika pamoja na Mikutano Mikuu ya Vijiji.

3.0. Uhakiki na uandikishaji wa Kaya masikini

Wakati wa utambuzi wa kaya masikini  zana iliyotumika ilikuwa ni dodoso ambalo mlengwa alihojiwa na taarifa zake zilichukuliwa na baadaye kuingizwa katika mfumo maalumu wa kompyuta, kunyambulishwa  na baadaye majibu yalitolewa kuonesha ni kaya zipi zilikidhi vigezo vya kuitwa kaya masikini. Kaya zilizokidhi vigezo ziliingizwa kwenye zoezi la uhakiki na kuandikishwa. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Vijiji vilivyomo katika mpango huu ni sitini na nne (64) sawa na asilimia 69% ya vijiji vya Msalala. Vijiji hivi 64 vina  jumla ya kaya 5813 zilizoandikishwa na zilizokuwa zinahudumiwa na Mpango huu wa Kunusuru Kaya Masikini mpaka Oktoba  2016.

Aidha lilifanyika zoezi la uhakiki wa kuondoa kaya zisizo kuwa na sifa ya kuendelea kuwa kwenye mpango, ambapo Halmashauri iliondoa kaya 153 na kubakia na kaya 5660 . Kaya hizi ziliondolewa kwa kuzingatia vigezo vya kifo,kuhama kusikojulikana, kuwa familia za viongozi na zingine kuonekana kuwa kaya zenye watu wenye uwezo. Hata hivyo zoezi la uhakiki wa kaya ni endelevu, kwa sasa Halmashauri inazo kaya masikini 5641 zinazolipwa fedha.

4.0. Uhawilishaj Fedha kwa Walengwa

Katika mwaka wa fedha 2015/2016 hadi 2017/2018   uhawilishaji wa fedha kwa kaya lengwa umeshafanyika kwa awamu kumi na nane, kwa maana kwamba kila mwaka kuwa na awamu 6. Katika kipindi chote hicho Halmashauri imepokee Tsh. 4,549,704,454.57 ikiwa ni fedha ya kaya masikini, ruzuku ya kijiji na fedha uwezeshaji na usimamizi wa malipo. Uhawilishaji fedha umefanyika  kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini:

Jedwali na 1 linaonesha fedha iliyolipwa kwa madirisha mawili

Na 
MWAKA
MAPOKEZI YA FEDHA 
1.
2015/2016

1,664,253,670.44

2.
2016/2017

1,476,120,112.13

3.
2017/2018

1,409,330,672.00

 
Jumla 

4,549,704,454.57

4.10. Utoaji Elimu kwa Jamii Siku ya Malipo

Kabla ya zoezi la ulipaji fedha kwa walengwa, wawezeshaji ngazi ya wilaya hutoa mafunzo kwa walengwa, kupitia vipindi vya mafunzo kwa jamii kwa   wajumbe wa kamati za usimamizi, wenyeviti wa vijiji na watendaji wa vijiji. Mafunzo yatolewayo kati vipindi hivi ni pamoja na kuwahimiza walengwa kutimiza masharti ya kukidhi vigezo vya elimu na Afya. Wawezeshaji pia uelimisha walengwa juu ya matumizi sahihi ya fedha wanazopata kama ruzuku za kunusuru kaya masikini. Kupitia mafunzo haya kuna walengwa ambao wameanzisha miradi midogo midogo ya ufugaji wa kuku, ufugaji wa mbuzi, kilimo cha bustani na hata wengine wameweza kukodisha mashamba na kununua mbegu bora na mbolea kwa ajili ya kuboresha kilimo.

4.20. Kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii

Katika halmashauri ya wilaya ya Msalala yenye jumla ya walengwa 5641 waliopo katika mpango wa kunusuru kaya masikini kwa sasa, kaya 3,731 zenye jumla ya wanufaika 22,386 zimejiunga na mfuko wa afya ya  jamii katika kipindi hiki cha malipo. Idadi hii ni sawa na asilimia 66.14 ya kaya zilizoko kwenye mpango huu. Aidha kuna kaya ambazo zilizokuwa zimejiunga awali na zinaendelea kupata huduma kupitia mfuko huu. Hata hivyo zoezi la uhamasishaji wa walengwa juu ya mfuko huu unaendelea ni matarajio yetu kuhamasisha kaya zote zijiunge na mfuko huu.

4.30. Mafanikio yaliyopatikana

  • Kutokana na mfuko huu jamii imeweza kunufaika kwa miradi ya ufugaji wa ng’ombe,mbuzi, ujenzi wa nyumba zilizoezekwa kwa bati. Pia katika msimu wa kilimo walengwa wametumia kiasi cha fedha hizi  katika shughuli za kilimo.
  • Kaya 3,731 kujiunga na mfuko wa afya ya Jamii (CHF), hali itakayo wezesha walengwa wapatao 22,386 kupata huduma ya afya kwa mwaka  kupitia mpango huu.
  • Taarifa za uhawilishaji toka vijijini kufika ofisini kwa wakati
  • Fomu za marekebisho ya taarifa za kaya zimejazwa
  • Fomu za madai kwa maeneo husika zimejazwa na kuingizwa kwenye mfumo

Jedwali linaloonesha mafanikio ya kaya masikini baada ya kupokea ruzuku kwa kipindi cha Julai 2015 hadi Machi 2018.

JUMLA KAYA
NG’OMBE
MBUZI
KONDOO
NGURUWE
KUKU
BATA
KILIMO
BIASHARA
NYUMBA
CHF

5641

252

1783

489

66

2949

501

2930

457

958

3731

Mojawapo ya mafanikio kupitia picha ni kama ifuatavyo;-

Picha 1.Baadhi ya Walengwa wakipokea fedha katika kijiji cha  Kakola NA. 9.







 

Picha 2.Baadhi ya Walengwa waliofuga mifugo katika kijiji cha  Ndala , walinunua mifugo hii kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF III).

  






Picha 3. Baadhi ya Walengwa waliojenga nyumba  katika kijiji cha  Itogwanholo , walijenga nyumba kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF III).

 

 

  

5.0. Changamoto

 
  • Katika kipindi hiki cha masika, barabara nyingi zimekatika, kupelekea CMC wanaokuja benki kuchukua fedha kutumia usafiri wa pikipiki ambao ni aghali ukilinganisha na usafiri wa mabasi, hali iliyopelekea bajeti ya nauli kupungua  na hivyo kutumia fedha za ufuatiliaji.
  • Ubovu wa barabara kutokana na mvua nyingi umesababisha baadhi ya magari kukwama na kusababisha walengwa kutopata pesa siku iliyopangwa.
  • Walengwa baadhi kutofika katika vituo vya kutolea fedha kutokana na shughuli za kilimo zinazoendelea kwa kipindi hiki cha masika.
 
  • Kutokuwa na Mfumo wa kompyuta wa TASAF III (Management Information System) hii inasabaisha utendaji kazi kuwa mugumu.
 

6.0. Mikakati 

 
  • Kuendelea kuhamasisha walengwa kujiunga katika mfuko wa afya ya Jamii (CHF)
 
  • Kuendelea kuomba TASAF makao makuu kutufungia Mfumo wa kompyuta wa TASAF III (Management Information System)
 
  • Halmashauri (W) kujazia pale panapotokea upungufu wa fedha kutokana na kuongezeka kwa gharama kutokana na matengenezo ya gari kuwa makubwa na mengine yanayofanana na hayo.
  • Kuwasisitiza walengwa kufika eneo la malipo kwa wakati kwa mujibu wa kalenda
  • Kuomba serikali kuu kupitia TARURA kuweza kutengeneza barabara ili kuweza kupitika kwa urahisi.
 

7.0.Hitimisho:

 

Ili kufanikisha adhima ya Serikali ya kupambana na umasikini kupitia Mpango huu wa Kunusuru Kaya Masikini, ushiriki wa Serikali kwa ujumla wake ni jambo la msingi. Mpango huu ni mtambuka kwani unagusa sekta nyingi za  Kijamii  na Kimaendeleo. Ushiriki wa Sekta za Kilimo, Afya, Elimu,Mifugo, Maendeleo ya Jamii kwa kutaja chache, ni muhimu sana katika kufanya utekelezaji wa mpango huu uweze kutoa matarajio yaliyokusudiwa. Ushiriki wa viongozi ngazi zote katika kusimamia utekelezaji wa mpango huu, ni jambo la lazima ili kufanikisha mpango huu muhimu wa kupambana na umasikini.

 

        

    

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.