• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

imetumwa: September 9th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Bi. Rose Robert Manumba ameitaka jamii ya watanzania hasa wa Halmashauri ya Msalala kujenga mazoea ya kufanya mazoezi kwa ajili ya kuimarisha Afya zao,ushauri huu umetolewa Tarehe 08/09/2024 wakati wa kukabidhi zawadi kwa mshindi wa mashindano ya Mahona Cup ambayo hufanyika kila mwaka kwa kuzishirikisha Timu za mpira wa miguu za Kata za Mega, Segese, Shilela, Lunguya, Bugarama, Bulyanhulu, Chela na Timu moja kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe ambapo kwa mwaka 2024, Timu za Mguu Tageti na Segese namba 3 zote kutoka kata ya Segese zilifanikiwa kucheza fainali.

MKurugenzi Mtendaji huyo amempongeza NDG.Patrick Mahona Mdhamini wa mashindano hayo na wadau wengine waliounga mkono kufanikisha mashindano hayo na akaahidi kutoa ushirikiano
muda wote Taasisi yake itakapohitajika kufanya hivyo kwani michezo huimarisha afya,hukuza mahusiano baina ya rika mbalimbali,huleta ajira na kuimarisha ushirikiano na zaidi ya
hapo ndani ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi inasisitiza kukuza na kuibua vipaji kwa vijana wa Kitanzania kupitia michezo hivyo ni jukumu letu kuhakikisha dhana hii inatekelezeka
kwa vitendo.

Akimkaribisha mgeni rasmi wa hafla hiyo,diwani wa Kata ya Segese MHE.Joseph Manyara amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji kwa kukubali kuhudhuria hafla hiyo na kuomba jamii kuendelea
kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali ya awamu ya 6 kupitia viongozi wa Halmashauri na Kata kwa pamoja ya kuwezesha kuwaunganisha wadau mbalimbali ndani ya kata ya Segese
na kuwezesha mashindano hayo kufanyika kwa ukamilifu na akaomba wananchi kuendelea kukiamini Chama Tawala kwani mambo mazuri yanabuniwa na viongozi wabunifu.

Nae Mdhamini wa Mashindano hayo Bwana Patrick Mahona amewashukuru wadau mbalimbali waliomuunga mkono katika kuhakikisha mashindano haya yanafanikiwa na kuomba wadau zaidi kujitokeza
ili kuwezesha mashindano haya kupanua wingo na kufanyika kihalmashauri kwani zipo faida nyingi kupitia mashindano haya.Amezitaja baadhi ya faida kuwa ni kuwezesha watoto yatima na
wanaoishi katika mazingira magumu kuendelea na masomo kwa kuwalipia gharama zao za masomo ambapo wapo vijana 3 wanaendelea na masomo ya kidato cha tano na sita.Sambamba na hilo mashindano
hayo yameongeza mori kwa wanafunzi kufanya vizuri kimasomo na kuibua vipaji kwani Shule ya Sekondari ya Mwl.Nyerere imeshiriki mashindano hayo na kuibuka kuwa mshindi wa 3 kati ya Timu 32
zilizoshiriki kwenye mashindano ya Mahona Cup 2024.

Gharama zilizotumika katika maandalizi, zawadi na utekelezaji wa mashindano ya Mahona Cup kwa mwaka 2024 ni Tsh.7,538,000 na washiriki wa mashindano hayo wamewapongeza wananchi wa kata ya Segese
kwa kujitokeza kwa wingi katika kuangalia mashindano hayo na kujitoa kwa hali na mali kuchangia pale ilipobidi,hii inaonyesha umoja na kuhamasika kwa hali ya juu kuunga mkono michezo kwani michezo
ni furaha na wameomba Serikali, wawekezaji na wadau mbalimbali kuwekeza viwanja vya michezo ndani ya kata ya Segese ili kuwezesha kuongeza mapato ya Serikali kwani jamii ya Segese na Kata jirani
zinathamini sana michezo.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.