• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI LAPONGEZA JITIHADA ZA SERIKALI

imetumwa: March 3rd, 2018

BARAZA LA MADIWANI LAPONGEZA JITIHADA ZA SERIKALI

Baraza la Madiwani na Wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala limepongeza jitihada  zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano

inayoongozwa na Mhe. Dr John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kutoa maelekezo mazuri ya matumizi

ya fedha za Ruzuku ya maendeleo (LGDG). Kauli hiyo ilitolewa na Baraza la Madiwani lililoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo

Mhe. Mibako Mabubu ambaye aliongeza kwa kusema "ni wazi kuwa miradi viporo iliyoibuliwa na jamii miaka iliyopita itapata suluhu katika

awamu hii kwa kuwa fedha zinazoletwa na Serikali kuu  zimedhamiria kukamilisha miradi husika ili ianze kutoa huduma kwa wananchi".


Baraza hilo limefanyika leo tarehe 03.03.2018 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo. Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndugu

Simon Berege ameomba  Baraza lipendekeze miradi ambayo ina uhitaji mkubwa kwa jamii sajali na kuangalia umbali wa huduma hiyo kwa lengo

la kuwezesha wananchi kupata huduma karibu na maeneo yao. Amesema Serikali ya awamu ya tano imetenga jumla ya Tsh: 851,382,999.00 kwa

Halmashauri ya Msalala ambapo hadi kufikia mwezi wa sita mwaka huu fedha hii itaingia katika akaunti za Halmashauri na kwenda moja kwa moja

katika miradi iliyopendekezwa. Sambamba na hilo Serikali kuu imetenga Tsh: 1,121,288,000.00 kwa mwaka wa fedha ujao 2018/2019.


Kwa upande wao Wah. Madiwani walipokea taarifa hizo kwa furaha na kuahidi kutoa ushirikiano wa kutosha na kuzisimamia fedha hizo kikamilifu

katika maeneo yao ya utendaji ili kuweza kutekeleza lengo la Serikali. Baraza hilo lilipendekeza kukamilishwa kwa kituo cha Afya cha ngaya,

kukarabati miundo mbinu ya bomba la maji katika kata ya Segese, kujenga kituo cha kuzalishia mifugo katika kata ya Mega, Ukamilishaji wa

vyumba 12 vya madarasa katika kata za Mwakata na Kashishi, ukamilishaji wa nyumba 8 za walimu katika kata za Isaka, Busangi, Chela na Bulyanhulu,

ujenzi wa madarasa 3, nyumba 1 ya walimu na maabara 3 katika shule mpya ya Sekondari Kashishi. Shughuli hizi zitafanywa kwa fedha za mwaka huu

2017/2018 na miradi hii kuanza kutumika.


Kwa mwaka 2018/2019 Baraza hilo lilipendekeza shughuli za ukamilishaji na kuipandisha hadhi zahanati ya Isaka kuwa kituo cha Afya,

ukamilishaji wa majengo ya wagonjwa wa nje (OPD) katika kata za Mwanase, Mwalugulu na Busangi, Ukamilishaji wa vyumba 15 vya madarasa katika kata za

Lunguya, Segese, Mega, na Kashishi, na ununuzi wa ng'ombe 20, mbuzi 50 na kuku 500 . Hii ni baadhi ya miradi itakayotekelezwa.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.