• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI LAPONGEZA MAANDALIZI MAZURI YA BAJETI 2018/19

imetumwa: January 19th, 2018


Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Msalala limempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo pamoja na timu yake ya Wataalamu kwa kufanya maandalizi vizuri ya makisio ya bajeti kwa mwaka 2018/19. Maandalizi hayo yamewezesha wajumbe kusoma bajeti hiyo kwa urahisi na kutoa michango yao kwa ufasaha. Kikao hicho kimefanyika kwa muda wa siku mbili tarehe 19/01/2018 – 20/01/2018 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.

Akimkaribisha Mwenyekiti wa Halmashauri kufungua kikao cha baraza hilo kaimu Mkurugenzi (W) ndugu Masatu Mnyoro alisema Bajeti ya mwaka wa Fedha 2018/2019 imelenga kuongeza uwekezaji katika shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo ujenzi wa maegesho katika kata za Isaka na Bugarama  ili kuondoa utegemezi wa Halmashauri kutegemea mapato toka mgodi wa Bulyanhulu (ACCACIA),  ambapo awali mgodi huo ulichangia asilimia 75 ya makusanyo ya ndani ya Halmashauri.

Nae kaimu Afisa mipango (W)  ndugu Conchesta Kabete alisema kwa mwaka wa Fedha 2018/19 Halmashauri ya Msalala imepanga kukusanya na kutumia jumla ya Tsh: 36,505,636,440 kutoka katika vyanzo mbalimbali kama inavyoonekana:

Na.
Chanzo cha Fedha
Makisio 2018/2019
1.
Mapato ya Ndani
5,195,632,500
2.
Ruzuku ya Kawaida (OC)
854,860,000
3.
Ruzuku ya Mishahara
23,446,903,848
4.
Ruzuku ya Miradi ya Maendeleo
7,008,547,592

JUMLA
36,505,636,440

                                                                                                         

Sambamba na uwasilishaji wa Bajeti hiyo, Kaimu Afisa Mipango (W) huyo alisema bajeti hiyo imeandaliwa kwa kufuata miongozo mbalimbali ikiwemo Dira ya maendeleo ya Taifa, Mpango mkakati wa Halmashauri, Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi na sera mbalimbali za kisekta. Pia alitoa mrejesho wa bajeti ya mwaka wa Fedha 2017/2018 ambapo Halmashauri ilipanga kukusanya Jumla ya Tsh: 31,110,652,593 hadi kufikia mwezi wa kumi na mbili 2017 Halmashauri hiyo ilikusanya Tsh: 10,387,052,140.18 sawa na 33.5% ya makusanyo yake. Alitaja baadhi ya Mafanikio yaliyopatikana hadi mwezi Disemba 2017 kuwa ni ujenzi wa mabweni katika shule za Bulige na Ntobo, kuendelea kwa ujenzi wa jengo la makao makuu ya Halmashauri, kukamilika kwa mradi wa maji Igombe na Mhama kutoka bomba la Ziwa Viktoria, Kukamilika kwa miundombinu ya soko la kimkakati na ghala la kuhifadhia mazao ambalo lilifadhiliwa na MIVARF, kukamilika na kuanza kutumika kwa zahanati nne na kuendelea kwa taratibu za ujenzi wa Maji wa pamoja JWPP ambao umekusudia kupeleka maji katika kata ya Bugarama na Bulyanhulu, mradi huu takamilishwa ndani ya miezi 12 kuanzia Disemba 2017 na umefadhiliwa na Wizara ya maji, kampuni ya Accacia na Halmashauri ya Msalala.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Mibako mabubu alisema bajeti hiyo ni vema iangalie uwezekano wa kutatua changamoto mbalimbali za wananchi ikiwemo ukamilishaji wa maboma yaliyokwama kwa muda mrefu ambapo kaimu Mkurugenzi (W) ndugu Masatu Mnyoro aliahidi suala hilo kulifanyia kazi kwa kuwa tayari Halmashauri imepeleka maandiko sehemu mbalimbali kutafuta wadau wa kukamilisha miradi hiyo, suala hili liliungwa mkono na wah. Madiwani wote na Mh. Ezekiel Magolyo Maige aliomba kupatiwa maandiko hayo sambamba na kupewa taarifa za mara kwa mara juu ya miradi yenye changamoto ili aweze kushiriki kutafuta wadau mbalimbali wa kimaendeleo.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.