• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Baraza laridhia mapendekezo ya bajeti ya CSR

imetumwa: November 29th, 2023

Baraza la Halmashauri ya Msalala Wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga limeridhia na kupitisha mapendekezo ya Mpango wa uwajibikaji

wa Makampuni kwa jamii (CSR) kwa mwaka 2024.Kikao hicho kimehudhuriwa na waheshimiwa madiwani wote,mheshimiwa Mbunge,Wakuu wa

idara na Vitengo wa Halmashauri,wataalamu toka ngazi ya kata na vijiji,wawakilishi wa wataalamu toka idara ya maendeleo ya jamii

kutoka Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu na wananchi kwa ujumla.


Akiwakaribisha wajumbe katika kikao hicho,Mkurugenzi Mtendaji(W) NDG.Khamis Katimba ameeleza maagizo ya Serikali yaliyotolewa katika

kikao chao na Waziri wa ofisi ya Rais,TAMISEMI MHE.Mohamed Omar Mchengerwa kuwa Halmashauri nchini zinapaswa kuhakikisha zinatumia

mfumo mpya ujulikanao kwa jina la TAUSI katika kukusanya mapato kwani mfumo huu umeondoa changamoto za upotevu wa mapato kwa kuzimba

mianya yote ya udanganyifu wa mapato.


Pia Halmashauri zihakikishe miundombinu iliyowekwa na Serikali inakuwa na miundombinu yote inayotakiwa ili kuwezesha miradi kutoa

huduma kwa wananchi kwa wakati,ametaja miongoni mwa miundombinu hiyo kuwa ni uwepo wa madawati katika shule za msingi na sekondari

ambapo amesema katika halmashauri ya Msalala yanahitajika madawati 8,712 viti na meza 4,902 ambapo yeye yupo tayari kuhakikisha

upungufu huu unapatiwa suluhisho.Agizo jingine ni kushirikiana na kuhakikisha shughuli za Halmashauri zinatangazwa tokea ngazi za

vijiji.


Mkurugenzi huyo amewataka wajumbe hao kupendekeza miradi yenye tija kwa jamii zao kwani mpango huu ni maalum kwa ajili ya shughuli

za kuwezesha jamii kujiendeleza kiuchumi, ametaja maeneo ya kipaumbele yaliyotolewa na uongozi wa Barrick Gold Mine kuwa ni maeneo ya

afya ambapo amesema watu wakiwa na afya njema inawawezesha kuendelea na shughuli za uzalishaji uchumi,eneo lingine ni elimu ambapo

watoto wakipatiwa elimu bora huleta ukombozi baadae kwa familia na taifa kwa ujumla.


Akiwasilisha mpango na bajeti ya uwajibikaji wa makampuni kwa jamii (CSR) Afisa mipango na Uratibu(W) NDG.Elkana Zabron amesema kwa mwaka

2023 fedha za uwajibikaji wa Makampuni kwa jamii (CSR) Halmashauri ilipanga kutumia Tsh.1,977,800,000 katika sekta za Afya na Elimu ambapo

hadi sasa Halmashauri imetumia Tsh.1,350,399,442.24.Ameitaja baadhi ya miradi iliyotekelezwa kupitia fedha hizi kuwa ni ujenzi wa mabwawa ya kunyweshea

mifugo katika kata ya Bulyanhulu,ujenzi wa ofisi ya kata Bulyanhulu,kukamilisha jengo la utawala, vyumba 2 madarasa na matundu ya vyoo 8 katika

 chuo cha VETA kata ya Bugarama na ujenzi wa uzio stendi ya Isaka.


Kwa mwaka 2024 Halmashauri inatarajia kutumia Tsh.2,000,000,000.00 kutoka katika chanzo cha uwajibikaji wa makampuni kwa jamii(CSR) kinacholipwa na

mgodi wa barrick,Halmashauri ikishirikiana na wataalamu kutoka Kampuni ya Mgodi wa dhahabu wa Barrick-Bulyanhulu wamewezesha uibuaji wa vipaumbele.

Vipaumbele hivi vimezingatia muongozo wa uwajibikaji wa Makampuni wa mgodi huo ambapo utajikita kwenye maeneo ya uchumi na uzalishaji,Mazingira,

Kilimo na huduma za jamii ikiwemo elimu na afya.Aidha mpango huu utajikita katika kulipa madeni ya miradi iliyotekelezwa miaka ya nyuma na kutekeleza

 maagizo ya serikali ambapo Halmashauri imetenga Tsh. 400,000,000 kuwezesha madawati, viti na meza kupatikana na Tsh. 200,000,000 kwa ajili ya kuongeza

vifaa tiba na kuajiri wataalam 16 wa idara ya Afya kupunguza ukosefu wa wataalamu katika sekta hiyo.


Nae Mbunge  wa jimbo la Msalala Mhe.Alhaj Idd Kassim Idd ameitaka Halmashauri kuhakikisha mpango uliowasilishwa unatekelezwa kwa vitendo na kwa wakati

kwani fedha inayotolewa na Mgodi wa Barrick-Bulyanhulu si hisani bali ni takwa la kisheria kwa Kampuni hiyo kuwajibika kwa jamii inayoizunguka na akaipongeza

Halmashauri chini ya uongozi wa mwenyekiti Mibako Mabubu kwa kuongoza jamii kuibua miradi yenye mashiko kwa wananchi,ametaja baadhi ya maeneo ambayo Halmashauri

imepanga kufanyia kazi kuwa ni kuajiri wataalam wa afya kwenye maeneo ambayo Serikali haijapeleka wataalamu kwani Halmashauri imefungua zahanati 5 na mwezi

Januari 2024 itaongeza zahanati 8 na kupandisha hadhi zahanati za Segese na Bulige kuwa vituo vya afya.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita amempongeza Mbunge wa jimbo la Msalala kwa kuliwakirisha vema jimbo lake bungeni kwani kila kona ya

Halmashauri ya Msalala miradi ya maendeleo inatekelezwa kutokana na jitihada za Mbunge za kuiomba Serikali yetu tukufu inayoongozwa na Rais kipenzi cha watu

mama yetu Dr.Samia Hasain Suluhu na kuahidi kuendelea kushirikiana na uongozi wa Halmashauri hiyo kuwezesha ilani ya CCM kutekelezwa kwa ufasaha,ameongeza

kusema hana tatizo na Halmashauri hiyo kwani siku zote Halmashauri ya Msalala hutekeleza miradi ya wananchi kwa ubora na viwango vya juu hii yote inatokana

na uongozi thabiti wa Mwenyekiti wa Halmashauri na baraza lake bila kumsahau Mkurugenzi shupavu NDG.Khamis Katimba hakika unaupiga mwingi katika kuhakikisha

maagizo ya Serikali ya awamu ya sita yanatekelezwa kwa wakati.


Nao baadhi ya madiwani akiwemo Mhe.Shija diwani wa Kata ya Bulyanhulu ameitaka Halmashauri kutembelea maeneo yaliyopendekezwa kabla ya utekelezaji na kutengeneza BOQ inayoendana na uhalisia

wa bei za soko,suala ambalo limeungwa mkono na Mhe.Benedict Manwali diwani wa kata ya Lunguya na Mhe.Masanja diwani wa kata ya Mwanase ameipongeza mpango huo kwa kuwa wananchi wa kata yake

wanahangaika kufuata huduma katani hivyo uwepo wa zahanati nyingine utawezesha wananchi kupata huduma karibu.


Kikao hiki kimehitimishwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe.Mibako mabubu kumhakikishia Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe.Mboni Mhita kuwa maagizo na maelekezo yote yaliyotolewa na

Serikali ya awamu ya sita yanatimizwa kwa wakati kwani Mkurugenzi Mtendaji(W) na timu yake ya wataalam ni wasikivu na wachapakazi hivyo yale yote yaliyopitishwa kwenye mpango

wa CSR kwa mwaka 2024 yatatekelezwa na kuwaomba wananchi wa Halmashauri ya Msalala kuilinda na kuitunza miradi iliyokwisha tekelezwa kwani fedha ya Serikali ni fedha yao hivyo

tuithamini miradi yetu.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.