• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

BORESHENI VYANZO VYA MAPATO

imetumwa: January 11th, 2019

Kauli hii imetolewa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira Mhe. Gerard Mwanzia wakati wa kikao cha kujadili na kupitia bajeti kwa mwaka wa fedha 2019/20 katika ukumbi wa Halmashauri ya Msalala. Mhe, Mwanzia amesema kutokana na hali halisia ya mapato ndani ya Halmashauri ni vema vyanzo vya mapato vilivyopo vikaboreshwa Zaidi ili kuweza kuwa na uhakika wa kukusanya ushuru ambapo amesema katika bajeti hii Halmashauri ni lazima iweke bajeti ya kujenga uzio katika mnada wa Bulige, Masabi na baadae Bugarama.

Suala ambalo limetolewa ufafanuzi na mkuu wa idara ya Mifugo na Uvuvi DR. Ntanwa Kilagwile ambapo amesema bajeti imezingatia ushauri kwani katika mpango wa bajeti kwa mwaka 2019/20 Halmashauri imepanga kujenga uzio katika mnada wa Bulige na kuboresha miundombinu ya gulio la kakola sambamba na kufanya ukarabati wa majosho mawili. Halmashauri inalazimika kukamilisha ujenzi huo kidogo kidogo kutegemeana na upatikanaji wa Fedha.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Mipango (W) ndugu Elkana Zabron akitoa taarifa ya bajeti kwa wajumbe wa kamati hii amesema katika mpango na bajeti ya 2019/20 Halmashauri imepanga bajeti kulingana na hali halisi ya makusanyo yake kwani katika mwaka 2017/18 Halmashauri ilipanga bajeti kulingana na maoteo suala ambalo lilisababisha Halmashauri kuwa miongoni mwa Halmashauri zilizofanya vibaya katika ukusanyaji mapato hii ilitokana na kukadiria mapato yasiyokusanyika kutoka mgodi wa Bulyanhulu ambao ulipunguza uzalishaji na hivyo kuathiri mapato ya Halmashauri ambayo yalichangia Zaidi ya 75% ukijumlisha na ushuru unaolipwa na makampuni yanayofanya kazi na mgodi.

Wajumbe hao waliitaka Halmashauri ianze kupimia watu viwanja kwa kutumia makampuni kwani viwanja ni chanzo kingine kizuri cha mapato sambamba na kuwaomba TARURA kuchukua mahitaji ya matengenezo ya barabara kutoka Halmashauri kwani itasaidia kutatua maeneo korofi ya barabara kwa kuwa Halmashauri inatambua maeneo hayo.

Nae Mkurugenzi Mtendaji Bwana Simon Berege amesema tayari Idara ya Ardhi na Maliasili imeshaanza kupima viwanja katika kata za Ntobo, Mega na segese na Halmashauri inategemea kupata fedha toka wizara ya Ardhi na Maliasili kwa ajili ya upimaji wa viwanja ndani ya Halmashauri na hivyo itashirikisha makampuni ili maeneo mengi yaweze kupimwa, Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema pia Halmashauri ya Msalala ni miongoni mwa Halmashauri makini Tanzania kwani iliandaa maandiko mbalimbali ambayo Serikali iliziomba Halmashauri nchini ziandae kulingana na mahitaji yao ili Serikali kuu iweze kuleta fedha ya kukamilisha miradi hiyo hivyo tunategemea kupokea fedha za kukamilisha miradi mbalimbali ndani ya kata zetu.

IMETOLEWA NA KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO

MSALALA

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.