• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Elimu ya ukatili iwe ajenda ya kudumu

imetumwa: December 10th, 2023

Kauli hii imetolewa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kahama bwana Vicent Ndesekio wakati wa maadhimisho ya kilele cha siku 16 za kupinga ukatili

kilichofanyika Kiwilaya katika Kata ya Mwalugulu kijiji cha Igunda ambapo Bwana Vicent amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.

Rais Samia Suluhu kwa kuleta mabilioni ya fedha ndani ya Tarafa, ametaja baadhi ya miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa kipande cha reli ya kisasa

katika kata ya isaka ambapo wananchi wengi wameajiriwa, zaidi ya Tsh.bilioni 18 zimetumika katika kukamilisha mradi wa Umeme Vijijini (REA)

katika kata za Isaka,Jana na Mwalugulu ambapo amesema katika kata ya Mwalugulu vijiji vyote wamepitiwa na Mradi huo.


Bwana Vicent amempongeza Mbunge Alhaj Idd Kassim Idd kwa jitihada zake anazozifanya za kuwaletea maendeleo wananchi wa Msalala sambamba na kuunga mkono

jitihada za Mhe.Rais Samia Suluhu kwani mwaka 2021 alipeleka chuo wasichana 60 waliopata changamoto za kutomaliza masomo yao ya sekondari na kuwalipia

ada,2022 alipeleka wasichana 50 na mwaka 2024 atapeleka wasichana 60 na kuitaka jamii kuchangamkia fursa zinazotolewa na Mbunge wao. NDG,Vicent amemshukuru

pia Mkuu wa Wilaya ya Kahama  Mhe, Mboni Mhita kwa kuendelea kuimarisha ulinzi na usalama ndani ya Wilaya na kuetikia mialiko mbalimbali ndani ya Wilaya yenye

lengo la kutatua changamoto za kijamii.


Awali akimkaribisha Mgeni Rasmi,Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala ambaye pia ni diwani wa Kata ya Mwalugulu, Mhe.Frola Sagasaga amemshukuru Mhe. Rais

Samia kwa kutekeleza vema Ilani ya chama cha Mapinduzi kwani ndani ya Kata ya Mwalugulu miradi mingi imetekelezwa ikiwemo ujenzi wa kituo cha Afya Mwalugulu

ambacho kimekamilika na kinatoa huduma kwa jamii, Mradi wa Umeme Vijijini unaendelea kutekelezwa na kwa vijiji vya Igundu na Mwankima tayari unawaka japo kuna

changamoto za kiutendaji hivyo amemwomba mgeni rasmi kuwasiliana na Tanesco ili kuweza kutekeleza mradi huo kwa muda uliopangwa sambamba na kutatua changamoto

za wananchi katika vijiji vya Igundu na Mwankima.


Nae Kaimu Mkurugenzi Mtendaji(W) NDG.Judica Sumari amewashukuru wananchi wa Vijiji vya Igundu na Mwankima kwa kujitokeza kwa wingi kuhudhuria maadhimisho ya

kilele cha siku 16 za kupinga ukatili ndani ya Halmashauri ya Msalala ambapo amesema katika siku 16 wataalamu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii walitoa elimu

kwa jamii katika kata zote 18 za Halmashauri na kuongeza kusema jamii kwa kiasi kikubwa imeelimika kwani matukio ya kesi za ukatili kwa mwaka 2023 yamepungua

hivyo jamii imehamasika na ameahidi kuendeleza mapambano dhidi ya ukatili na kuwataka Watendaji wote ndani ya halmashauri kuweka ajenda ya kupinga ukatili wa

kijinsia kuwa ajenda ya kudumu katika vikao na mikutano yao yote na kuahidi kufuatilia kupitia Mihitasari ya vikao vyao.


Akisoma risala ya kilele cha maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili ndani ya Halmashauri ya Msalala, Mratibu wa kupinga ukatili kwa wanawake na watoto Bi,

Veronika Mfuko ameyataja mafanikio yaliyopatikana ndani ya Halmashauri ni kuundwa kwa kamati za kupinga ukatili wa kijinsia kwenye mikutaniko ya watu wengi

katika kata za Segese, Bulige na Bulyanhulu.Mafanikio mengine ni kufunguliwa kwa jengo shufwa(one stop center) katika kata ya Bugarama na kuanzishwa kwa huduma

ya dawati la Jinsia katika kituo cha Polisi Bugarama na watoto wa kike kujengewa uwezo wa kujiajiri kupitia mafunzo yaliyoyapata katika chuo cha ufundi stadi cha

mt.Francis kilichopo katika kata ya Mwakata.Pia ametaja ufinye wa bajeti kuwa ni kikwazo kikubwa katika utekelezaji wa shughuli za kitengo cha kupinga ukatili wa

kijinsia na kuomba changamoto hii kupatiwa ufumbuzi.


Kwa upande wao wananchi wa Vijiji vya Igundu na Mwankima wamemshukuru Mgeni rasmi kwa kuthamini mwaliko wao na kuja kusherehekea pamoja kilele cha Maadhimisho hayo

na kumwomba kutembelea vijiji hivyo mara kwa mara na kuona shughuli za wananchi hao ambao wengi wao ni wakulima wa Mpunga na kuiomba Serikali na wadau wa maendeleo

kuchangamkia fursa za uwekezaji kwa kujenga mashine za kukoboa ndani ya eneo hilo kwani kwa sasa umeme upo, hii itawasaidia kutosafirisha mazao yao kwenda Kagongwa

na hivyo kuongeza mapato kwa Halmashauri ya Msalala.Suala hili limechukuliwa na Mkurugenzi Mtendaji(W) na kuona namna ya bora ya kulifanyia kazi kwani Mkurugenzi huyo

anakutana na wadau mbalimbali nchini hivyo itakuwa rahisi kwake kufikisha taarifa hii njema kwa Taifa.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.