• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Halmashauri yadharimia kuongeza makusanyo mapato

imetumwa: June 27th, 2024

Halmashauri ya Msalala Wilayani Kahama imeweka malengo ya kukusanya Tsh. Bilioni 7 katika mwaka mpya wa fedha 2024/25 ambapo kwa mwaka uliopita ilikusanya Tsh. Bilioni 6 na milioni 300 na kuvuka

lengo la kukusanya Bilioni 5.7 ambapo imekusanya zaidi ya milioni 600 hadi kufikia leo tarehe 27.06.2024.Takwimu hizi zimetolewa na Mkurugenzi Mtendaji(W) bwana Khamis Katimba wakati wa kikao cha

kufanya Tathmini ya mwaka wa fedha 2023/24 na kuweka malengo kwa mwaka ujao 2024/25.


Kikao hicho kimejumuisha Katibu Tawala wa Wilaya ya Kahama,Maafisa Tarafa wa Tarafa za Msalala na Isagehe,Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri,Watendaji wa kata na vijiji wote wa Halmashauri hiyo.

Lengo la kikao ni kutathmini yaliyofanyika mwaka 2023/24 na kuweka malengo kwa mwaka 2024/25 sambamba na kukumbushana wajibu wa watumishi wa umma kwa jamii wanazoziongoza.Katika kikao hicho mada mbalimbali

zimewasilishwa zikiwemo ukusanyaji mapato,utawala bora,mipango na bajeti na maandalizi ya uchaguzi wa wenyeviti.


Bwana Katimba amesema mapato ndio uti wa mgongo wa Halmashauri na sisi ndio injini ya kuhakikisha mapato halali ya Halmashauri yanakusanywa,hakikisheni mianya yote ya upotevu wa mapato ya Halmashauri

inazibwa na fedha inakusanywa,sina shaka na ongezeko la bajeti tulilopatiwa kwani kupitia vikao ninavyovifanya mara kwa mara nanyi,wenyeviti wa vijiji na vitongoji na Waheshimiwa madiwani.Nina uhakika

Bilioni 6.7 zinakusanyika nami naongeza milioni 300 ili tukusanye Bilioni 7.


Nae Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu NDG.Mang'era amewataka watumishi kuwa wabunifu kwa kuweka na kusimamia kikamilifu mpango na bajeti ili miradi itakayopitishwa ngazi za kata ziwe na tija katika utekelezaji

wake kwani wao ndo wataalamu katika maeneo yao hivyo watumie elimu zao kuleta mabadiliko chaya ndani ya kata na Halmashauri kwa ujumla.Tumefanya vizuri mwaka huu tunaoumaliza siku si nyingi naomba

changamoto zilizojitokeza iwe fundisho kwa mwaka ujao ili tufanye vizuri zaidi na simamieni miradi yote inayotekelezwa penye changamoto tuwasiliane mapema.


Kwa upande wake Mkuu wa idara ya Utumishi na Raslimali watu NDG.Mary Nziku amewataka watumishi ndani ya Halmashauri kufanya kazi kwa bidii na kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya sita Inayoongozwa na

DR.Samia Suluhu na kutaka kero zote zitatuliwe kwa wakati kwani sisi tu karibu na jamii,hakikisheni vikao vyote vya kisheria vinafanyika na mihtasari ya vikao hivyo zinaletwa Halmashauri,Mkurugenzi ameweka mlezi

kwa kila Kata lengo ni kuhakikisha yanayojadiliwa katika maeneo yenu yanafika Halmashauri kwa wakati na Halmashauri kuyafanyia kazi kwa wakati.


Akihitimisha kikao hicho,Katibu Tawala Bi.Jackline amewataka watumishi kufuata sheria,kanuni na taratibu katika utendaji kazi wa kila siku ili kuepusha migogoro isiyokuwa na ulazima,fuateni miongozo katika

ukusanyaji mapato sambamba na kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa kwa watendaji wa vijiji pindi watakaposimamia ofisi za vijiji pasipo kuwa na wenyeviti wa vijiji.Mwaka huu tuna uchaguzi wa wenyeviti wa vijiji

na vitongoji hamasisheni wananchi kujitokeza kuboresha taarifa zao na baadae kujitokeza kwa wingi kuchagua viongozi wanaowahitaji kwa kuwa ni haki yao kuchagua viongozi.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.