• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Jamii yaaswa kuzingatia makuzi ya mtoto

imetumwa: December 4th, 2023

Imeelezwa na kusisitizwa mtoto ni lazima anyonyeshwe muda wa miaka 2 na kupatiwa vyakula vyenye mchanganyiko wa makundi yote yq vyakula

vikiwemo wanga,protini,matunda,mbogamboga,sukari kiasi na mafuta mara 5 kwa siku ili kuwezesha ukuaji wake na kumuondolea uwezekano wa kushambuliwa

na magonjwa,kauli hiyo imetolewa na Afisa Lishe mkoa wa Shinyanga Bwana Yusuph Hamis wakati wa kikao cha kujadili mpango na bajeti wa Kamati yaLishe ya

Halmashauri ya Msalala.


Awali akifungua Kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji(W) NDG.Khamis Katimba amewaomba wajumbe kufuatilia kwa makini mafunzo hayo kwani baada ya muda si mrefu

yatatumika katika mipango na bajeti ya Halmashauri,pia lishe ni suala mtambuka ambalo kila mtu anapaswa kufahamu kwa undani na kufanyia kazi kwenye

familia au jamii inayomzunguka.Tutaendelea kutoa fedha kwa ajili ya kuwezesha elimu kutolewa kwa jamii kwani ndani ya Halmashauri yetu naona mila na

desturi zina nguvu na kusababisha watoto chini ya miaka 5 kutopewa haki zao za msingi na hivyo kupelekea udumavu.


Akiwasilisha Mpango na Bajeti wa lishe kwa mwaka 2024-25,Afisa Lishe wa Halmashauri ya Msalala Bi,Mwamini Mziray amesema jamii imehamasika juu ya unyonyeshaji wa watoto

chini ya miaka 5 na kuomba kutilia mkazo suala la kula mbogamboga na matunda hasa kwa kinamama na watoto kwani kumekuwepo na changamoto ya upungufu wa

damu na matumizi ya chumvi isiyokuwa na madini joto hivyo ameiasa jamii kuhifadhi chumvi yenye madini joto sehemu salama mara baada ya kuifungua na kuitumia.

Sambamba na hili ametoa wito kwa shule kuendeleza kilimo cha mbogamboga na mahindi-mpunga ili kuwezesha wanafunzi kupata chakula cha asubuhi na mchana.


Bi,Mwamini Mziray amesema Mpango na Bajeti kwa mwaka 2024-25 umelenga kutatua changamoto zilizoonekana kwa mwaka 2023-24 na kuomba kwa pamoja kushirikiana

katika kuhakikisha elimu na mafunzo kwa vitendo yanatolewa katika maeneo yote ya utawala ndani ya Halmashauri kupitia warsha kwa jamii,vyombo vya habari na

kuwatumia wahudumu wa afya ngazi ya jamii kwani wana mchango mkubwa katika kufanikisha shughuli hii kwa kuwa wapo karibu na jamii na huishi maeneo ya jamii.


Masuala ya kupunguza utapiamlo,uzito mkubwa,upungufu wa madini kama Vitamini A,matumizi ya vyakula vilivyoongezewa lishe,matibabu kwa waathirika wa utapiamlo

yatolewe hasa katika vituo vya afya viongezwe ili waweze kupatiwa matibabu na kujenga mazingira wezeshi kwa wataalam kuweza kutembelea maeneo yenye changamoto.

Washiriki wametoa rai kwa wawezeshaji kutekeleza mpango wao kama ulivyo na kuahidi kutoa ushirikiano na kuomba watumishi waliopo ngazi za kata na vijiji washirikishwe

suala ambalo limekubaliwa.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.