• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa akagua Mradi Bulige

imetumwa: September 19th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe.Christina Mndeme leo amekagua na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa kituo

cha Afya Bulige,ambapo jumla ya majengo 6 yatajengwa.Majengo yaliyokamilika mpaka sasa ni Jengo la mama na mtoto,jengo

la upasuaji,jengo la maabara na jengo la wagonjwa wa nje na kubakiza majengo mawili ya wodi ya mama na watoto na nyumba

ya mganga mfawidhi.Mradi huo hadi kukamilika utatumia Tsh.Milioni mia tano,fedha ambazo zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania Dr.Samia Hasain Suluhu kuhakikisha afya za watanzania zinalindwa.


Mkuu wa Mkoa huyo ameridhishwa na hatua zilizofikiwa na kuitaka Halmashauri kukamilisha mapema ili huduma za afya zianze

kutolewa na amempongeza Rais Samia Suluhu kwa kuwathamini wananchi wa kipato cha chini kwani uwepo wa kituo hiki kitapunguza

gharama za kusafiri kufuata huduma sambamba na kuwezesha wananchi kuendelea na shughuli za uzalishaji mali kwani kimeokoa muda.

Awali akisoma taarifa ya kituo hicho mganga mfawidhi,Dr.Kihoza amesema kituo hicho kitahudumia zaidi ya watu 39400 kwani Bulige

imezungukwa na wachimbaji wa madini toka Halmashauri ya Shinyanga vijijini na hupata huduma Bulige.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya Msalala Mhe.Mibako Mabubu amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kumfikishia shukrani

Rais Samia Suluhu kwa kuitengea fedha halmashauri kiasi cha bilioni 7 kwa mwaka 2023-24 kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo

ndani ya halmashauri na kuahidi kukamilisha miradi hiyo kwa viwango vinavyotakiwa na kwa wakati ili kuunga mkono matarajio ya serikali

ya awamu ya sita.Nae Mwenyekiti wa CCM(W) Mhe.Thomas Myonga amewataka wananchi wa kata ya Bulige na Watanzania kwa ujumla kutopotoshwa

na wanasiasa wanaotaka madaraka pasipo matendo kwani Serikali inayoongozwa na CCM inatekeleza vizuri ilani yake kwa kusikiliza kero

za wananchi na kuzitatua hivyo kwa pamoja tumuunge mkono Rais wetu kwa kufanya kazi kwa bidii.


Katika Mkutano wa hadhara,Mkuu wa mkoa ametoa nafasi kwa wananchi kuuliza maswali au kuelezea changamoto zinazowakabili wananchi wa

kata ya Bulige ambapo wananchi wengi wamejitokeza na kuelezea changamoto walizonazo, baadhi ya changamoto zilizowasilishwa ni pamoja

na uwepo wa kusuasua kwa umeme suala ambalo mratibu wa umeme vijijini(REA) amelitolea ufafanuzi kuwa inatokana na maboresho yanayofanywa

na Tanesco kuongeza uzalishaji wa umeme nchini,katika suala hili Mkuu wa Mkoa ameitaka Tanesco kutoa ratiba kwa wananchi ili wafahamu

mda umeme utakuwepo au kutokuwepo.Suala lingine lililoulizwa ni uwepo wa fedha 10% kwa wanawake na vijana pia huduma ya mfuko wa afya

ya jamii(CHF).Changamoto hizi zimetolewa ufafanuzi na Mkurugenzi Mtendaji(W) NDG.Khamis Katimba ambapo amesema fedha ya 10% ni mkopo

usiokuwa na riba unaotolewa kuwezesha wanawake,vijana na walemavu kuwekeza kwenye shughuli mbalimbali na baada ya mda kurejesha,takwimu

zinaonyesha watu wengi hawarejeshi hivyo kuomba walionufaika kurejesha fedha hizo kwa wakati ili wengine wakopeshwe.CHF ni bima inayowezesha

kaya kupata huduma za afya kwa kaya kuanzia mtu mmoja na ukomo wake watu sita kwa kipindi cha mwaka mmoja,hivyo jamii jiungeni kurahisha

matibabu.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.