• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA WILAYA AWATAKA WAZAZI KUWEKEZA KWENYE ELIMU

imetumwa: January 5th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kahama ndugu Anamringi Macha leo amewataka wazazi kuwekeza kwenye Elimu kwa kuwawezesha watoto wao kwenda shule kwa kuwanunulia madaftari, nguo za shule na viatu sambamba na kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa kwani matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya Msingi uliofanyika mwaka jana Halmashauri ya Msalala watoto wamefaulu kwa 76.63% na hivyo kuleta changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa 73 ndani ya Halmashauri hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama amesema hayo katika kikao kazi kilichowakutanisha Mkurugenzi Mtendaji (W), Kaimu Afisa Elimu bwana Seleka Ntobi, Afisa Taaluma Sekondari, Katibu Tarafa , watendaji wa kata za Bulige, Chela, Busangi , Mwanase na Kashishi, Waheshimiwa Madiwani wa kata hizo, watemi wa sungusungu, wenyeviti wa vijiji na watendaji wa vijiji. Kikao hiki kimefanyika katika kata ya Bulige ambapo lengo la kikao kazi hiki ni kujadili namna ya kukabiliana na upungufu wa vyumba vya madarasa uliopo ambapo mkuu wa Wilaya amesema Halmashauri ifanye jitihada zake zote kuhakikisha watoto wote waliofaulu mtihani wanapata nafasi za kujiunga na kidato cha kwanza na kuwaomba Wah. Madiwani kufikisha ujumbe kwa wananchi ili wachangie nguvu zao kwa kujenga maboma na Serikali imalizie lengo ni kuwawezesha watoto wetu waliofaulu mtihani kuendelea na masomo. Ninawaomba wananchi “ Jengeni maboma na sisi Serikali tumalizie ili watoto wetu wasome”.

Akisoma taarifa ya ufaulu mbele ya mwenyekiti wa kikao kazi hicho Kaimu  Afisa Elimu Sekondari (W) amesema jumla ya wanafunzi 4935 walifanya mtihani waliofaulu na kuchagiliwa kujiunga na kidato cha kwanza ni wanafunzi 3717 sawa na 76.63% kati yao 19 wamechaguliwa kwenda nje Halmashauri ya Msalala. Hivyo kuna upungufu wa vyumba vya madarasa 73 kwa Halmashauri nzima, pia pana upungufu wa meza na viti, matundu ya vyoo hivyo naomba kila kiongozi aone namna ya kufanya ili tuweze kutekeleza agizo la mkuu wetu wa Wilaya kwani elimu ndiyo ufunguo wa maisha.

Nae Mkurugenzi Mtendaji (W) ndugu Simon Berege amesema ukamilishaji wa maboma utaangalia sehemu ambapo wananchi watakapokuwa wameonyesha jitihada zao kwakukamilisha boma/maboma mapema na kuahidi Halmashauri kukamilisha maboma hayo haraka ili yaanze kutumika na ametoa muda wa miezi miwili hadi kufikia mwezi wa tatu wanafunzi wawe tayari ndani ya madarasa hayo. Amewataka viongozi hao kuwa mabalozi wazuri kwa wananchi ili wawezekuchangia ujenzi huo wa maboma sambamba na kuomba mashirika ya dini na yasiyoya kidini, wadau mbalimbali kujitokeza kuchangia jitihada hizi kwani elimu ni urithi pekee kwa familia nyingi hasa zenye kipato kidogo.

IMETOLEWA NA KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO

MSALALA

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.