• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali Yapania Kuondosha Utegemezi

imetumwa: December 19th, 2022

Serikali katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga imejipanga kuondokana na utegemezi wa mapato yake

ya ndani kutegemea uzalishaji wa madini ya dhahabu unaofanywa na mgodi wa Bulyanhulu, kwani Halmashauri hiyo hupata 70% ya

mapato yake kutoka mgodi huo na 10% kutoka kwa wachimbaji wadogo wadogo. Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri

ya Msalala MHE. Mibako Mabubu wakati wa

ziara ya kujifunza namna ya uzalishaji wa zao la korosho katika Halmashauri ya Manyoni iliyoko mkoani Singida.


Ziara hiyo imeongozwa na Mhe. Mibako mabubu akiongozana na Baraza la waheshimiwa Madiwani, Mkurugenzi Mtendaji (W ) ndugu

Charles Fussi, na wakuu wa idara 6 wanaohusiana na shughuli za maendeleo na ustawi wa Halmashauri. Uchumi wa wananchi  wa

Halmashauri ya Msalala unategemea sana uchimbaji wa madini ya dhahabu unaofanywa na mgodi mkubwa nchini wa Bulyanhulu pamoja

na wachimbaji wadodo wadogo huku makusanyo mengine kama ushuru wa mazao, leseni za biashara na magulio yanachangia 20% kwenye

pato la Halmashauri.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji ndg. Charles Fussi amesema ardhi ya Halmashauri ya Msalala inafanana na ardhi iliyopo manyoni

hivyo wananchi wa Msalala wachangamkie fursa hiyo pindi Halmashauri itakapoanzisha uzalishaji kwani zao la korosho lina manufaa

makubwa kwa jamii, nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Manyoni katika salamu zake kwa wanamsalala amesema zao la korosho huanza kutoa

korosho ndani ya miaka 3 na huendelea kwa muda wa miaka 30 na zaidi. Zao hili likitunza vizuri huwa na kipato cha uhakika katika

kaya.

Akitoa maelekezo kwa waheshimiwa Madiwani na wataalamu,  Afisa Kilimo Halmashauri ya Manyoni bwana Kizenga Shaban amesema Halmashauri

ya Manyoni huotesha miche ya Korosho katika vitalu kwa muda wa miezi 3 na baadae huwauzia wananchi kwa Tsh. 1000 na kuwafuatilia wakulima

muda wote kwa lengo la kutoa ushauri wa kitaalamu katika uzalishaji wa zao hilo ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojito

keza. Halmashauri ya Manyoni imehusisha wadau mbalimbali waliopo ndani na nje ya nchi katika ulimaji wa zao hili hivyo ni vema pindi

uzalishaji uanzapo Halmashauri itoe matangazo kwa wadau ili kuunga mkono kilimo hicho.

Imetolewa na kitengo Cha Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Msalala.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.