• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YAPONGEZA JITIHADA ZA MAENDELEO MSALALA

imetumwa: July 18th, 2018

Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania imeupongeza uongozi wa Halmashauri ya Msalala

ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Simon Berege na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo MHE.

Mibako Mabubu kwa kazi nzuri zinazofanyika katika Halmashauri hiyo. Pongezi hizo zimetolewa

leo tarehe 16/07/2018 na Waziri Mkuu wa Tanzania MHE. Majaliwa Kassim Majaliwa wakati wa ziara

yake ya kikazi ndani ya Halmashauri hiyo.


MHE. Kassim Majaliwa amesema MHE. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli

anatambua kazi nzuri zinazofanywa na wafanyakazi wa Halmashauri ya Msalala na timu nzima ya Baraza

la Madiwani, na ndiyo maana anaunga mkono jitihada hizo kwa kuboresha huduma za Afya katika Halmashauri

hiyo ambapo kwa mwaka 2017/18 Serikali ilitoa Milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya mama na mtoto,

Maabara ya kisasa,  jengo la upasuaji, jengo la kuhifadhia maiti na nyumba ya Daktari katika kituo cha

Afya Chela. kazi ambayo Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ndg. Simon Berege, watumishi wake na Baraza la

madiwani wameifanya kwa kiwango cha juu cha ubora.


MHE. Kassim Majaliwa ameweka jiwe la msingi katika mradi huo ambao  tayari umeanza kutumika, MHE. Waziri Mkuu

ameomba Halmashauri iangalie uwezekano wa kupanua eneo la kituo hicho kwani kimepakana na makazi ya wananchi. Serikali

katika mwaka huu 2018/19 imetoa milioni 400 kwa ajili ya ujenzi kama huo uliofanyika lakini awamu hii ujenzi huo

utafanyika katika kata ya Ngaya ambapo zahanati ya Ngaya imepandishwa hadhi na kuwa kituo cha Afya kwani zahanati

hiyo hupokea wagonjwa kutoka kata za Kashishi, Bulige, Mwanase, na maeneo ya Halmashauri jirani za Shinyanga vijijini

na Kahama Mji. Nae Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dr. Thom Mtoi amethibitisha kuwa tayari kiasi hicho kimepokelewa

katika akaunti za halmashauri na kwa sasa wapo tayari kuanza utekelezaji wa ujenzi huo.


Mkurugenzi Mtendaji ameishukuru Serikali kwa kuleta fedha kwa wakati na ameahidi kuanza utekelezaji mapema, na kwa upande

wao wananchi wameipongeza Serikali kwa kuwathamini kwani kumekuwa na maboma mengi ndani ya Halmashauri ambayo yanahitaji

Serikali kumalizia ili yaanze kutoa huduma hivyo kuleta pesa na kuipandisha hadhi zahanati ya Ngaya kutasaidia kutatua kero

ya huduma ya Afya kwani wananchi wengi walitegemea kwenda kahama kupata huduma hivyo uwepo wa kituo cha Afya Ngaya kutasaidia

kupunguza gharama za kusafiri.


Imetolew na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Halmashauri ya Msalala.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.