• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

watumishi watiwa msasa kuboresha utendaji

imetumwa: February 29th, 2024

Watumishi wa Halmashauri ya Msalala Wilayani Kahama wa kada ya utawala ikijumuisha watendaji wa kata 18 na watendaji wa vijiji 92 wamepatiwa mafunzo yenye lengo la kuboresha

utendajikazi wao wa kila siku ili kuweza kuwahudumia wananchi kwa weredi na ufanisi mkubwa na kupunguza kero kwa wananchi.Mafunzo haya yametokana na maelekezo ya waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais

Tawala za Mamlaka za Mikoa na Serikali za Mitaa ( OR TAMISEMI) Mhe. Mohamed Mchengerwa aliyoyatoa kwa Wakurugenzi wote nchini kuhakikisha watumishi wanapatiwa mafunzo na semina mbalimbali ili

kuwaongezea ujuzi katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku.


Mafunzo haya yamefunguliwa na Mkurugenzi Mtendaji(W) NDG.Khamis Katimba ambaye amewataka watendaji hao kuhakikisha wanatenda haki kwa wananchi wanaowahudumia na kuhakikisha wanawashauri vizuri viongozi

waliopo katika maeneo yao ya kazi na kuwasimamia watumishi waliopo katika kata na vijiji vyao, masuala haya yote yatawezekana iwapo watendaji hao watakuwa mfano kwa watumishi wengine kwa wao wenyewe kufika

ofisini kwa wakati na kutoka saa 9.30 alasiri sambamba  na kuwa na lugha yenye staha kwa wateja wanaokuja kupata huduma katika ofisi zao.


Mkurugenzi Mtendaji huyo ameongeza kusema nakutana nanyi mara kwa mara lengo langu kubwa ni kuhakikisha mnaweza kujiendesha wenyewe na kuwaza nini utaifanyia Halmashauri yako na nchi yako kwa ujumla hivyo

tunapokutana kila mtu ana uwezo wa kutoa utaalamu na uzoefu katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku hivyo kuwa rahisi kwa wengine kujifunza kwani mnakutana na changamoto mbalimbali hivyo tunapokutana

tunabadilishana uzoefu na kuimarishana.Natumia gharama kubwa ili kuhakikisha mnasimama na ni matumaini yangu kuwa kero zilizo ndani ya uwezo wenu zinatatuliwa na panaposhindikana tuwasiliane.Simamieni mapato na

kuhakikisha fedha za serikali zinakusanywa ndo maana watendaji wa kata wote nimewapa pikipiki fanyeni ziara za kustukiza ndani ya vijiji ili kuongeza uwajibikaji kwa watumishi wengine nami ntapita kuona hili likitekelezwa

na pale inapoonekana pana uzembe ntachukua hatua,zingatieni tunayoyaelekeza.


Miongoni mwa mada zilizowasilishwa katika kikao kazi hicho ni  majukumu ya Mtendaji wa Kata na Kijiji,Vikao vya kisheria vinavyopaswa kufanywa ngazi ya kijiji na kata,chimbuko la Mamlaka za serikali za mitaa na sababu za

kuanzishwa kwake,Dhana nzima ya utawala bora,ukusanyaji mapato na sababu za msingi za kisheria za kwa nini malmaka za Serikali za mitaa zikusanye mapato, masuala ya TASAF na fursa zijazo kwa ajili ya machinga kwani Mhe.Rais

Samia Hassan Suluhu ameelekeza machinga wote kusajiliwa na kutambuliwa hivyo kotoa wito kwa machinga wote kufika ofisi za watendaji wa vijiji kupata maelekezo ya namna ya kujisajili. Mada hizi zimewasilishwa na Mwanasheria wa

Halmashauri wakili msomi Leonard Mabula akishirikiana na mkuu wa idara ya utawala na Usimazi wa rasilimali watu Bi.Mary Nziku ambaye amewataka wana semina kuthamini nafasi walizonazo na kuzitumikia kwa bidii ili kuleta tija ndani

ya halmashauri na kuongeza uwajibikaji na uwazi kwa jamii ambalo ndilo tarajio kubwa la Serikali yetu tukufu ya awamu ya sita.


Kwa upande wao wanasemina,wamepongeza jitihada za Mkurugenzi Mtendaji (W) kwa kuwaamini na kukaa nao mara kwa mara kwani tangu aripoti ndani ya halmashauri semina hii ni tatu ambayo inafanyikia katika jengo la Makao makuu ya Halmashauri

iliyopo katika kata ya Ntobo,pia NDG.katimba amekuwa akitembelea kata na vijiji mbalimbali kila wiki na kukutana na watumishi wa kada za Elimu Msingi na Sekondari,Afya,Kilimo mifugo na umwagiliziaji na kuwakumbusha wajibu wa kazi zao na matarajio

yake kwao."Hongera sana kiongozi wetu nasi hatutakuangusha" kauli hii imetolewa na NDG.Patrick Mahona mtendaji wa kata ya Segese, kwani sasa hivi tunahudhuria vikao vya baraza la madiwani na kuwasilisha taarifa zetu za utekelezaji,suala ambalo linatujengea

uwezo wa kusimama popote.Nae Bi Neema magwega mtendaji wa kijiji cha Ntambalale ameishukuru Halmashauri kwa kutoa mafunzo kwa mabaraza ya ardhi ya kata kwani migogoro mingi iliyopo vijijini ni masuala ya ardhi hivyo sisi kama watendaji wakuu tutayasimamia kwa

ukamilifu na kuhakikisha haki inatendeka.


Mafunzo haya yamehitimishwa na Mkurugenzi Mtendaji(W) NDG.Katimba kwa kuwahakikishia watendaji hao kuwapa Tsh.200,000 kwa kila kijiji na kata kila robo mwaka kwani bajeti hiyo imepagwa,fedha hizi zitumike kununulia vitendea kazi vya ofisi.Pia ntaendelea kuwezesha

mafunzo ya muda mfupi na mrefu nanyi jengeni tabia ya kujiongeza kwa kujisomea mambo mbalimbali ikiwemo miongozo inayotolewa na serikali ili kuongeza upeo wa kujua mambo mengi na kukurahisishia utendaji kazi wako.Simamieni miradi na miundombinu ili kuhakikisha inakamilika kwa ubora

unaotakiwa na mwisho fanyeni mikutano ya kisheria kama inavyotakiwa.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.