• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Baruapepe za watumishi |
Msalala District Council
Msalala District Council

Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Mawasiliano Serikalini
    • Idara
      • Aridhi na Nyumba
      • Maendeleo ya jamii
      • Mipango Takwimu na Tathimin
      • Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Maji
      • Ujenzi na Miundombinu
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Utalii
    • Kilimo
    • Misitu
    • Ufugaji Nyuki
    • Viwanda
    • Usafirishaji
    • Michezo na Burudani
    • Ufugaji
    • Biashara
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Kukodisha Mitambo
    • huduma za Afya
    • huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Animal Keeping
    • Kilimo
    • Huduma kwa Watumishi
    • Tasaf
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Ratiba
      • Councillors meeting
      • Chairperson Appointment
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Finance and Planning Committee
      • HIV Committee
      • Health and Education Committee
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyoidhinishwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Hatua
      • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Ripoti
    • Mpango mkakati
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Matukio Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI MKUU AKATA MZIZI WA FITINA UJENZI WA KIWANDA CHA BOMBA LA MAFUTA

imetumwa: July 14th, 2018


Leo tarehe 14/07/2018 ziara ya kikazi ya siku 4 Wilayani Kahama imeanza rasmi ambapo Waziri mkuu MHE. Majaliwa Kassim Majaliwa amepokelewa na umati mkubwa wa wananchi wa Kata ya

Isaka katika Halmashauri ya Msalala, umati huo umeongozwa na Mbunge wa jimbo la Msalala MHE. Ezekiel Maige, Mkuu wa Wilaya ya Kahama ndg. Fadhir Nkurlu, Mkurugenzi Mtendaji

Halmashauri ya Msalala na Viongozi mbalimbali wa chama na Serikali. Wilaya ya Kahama ina Halmashauri 3 ambazo Waziri mkuu atazitembelea na kuzindua miradi mbalimbali za maendeleo


Akimkaribisha Waziri mkuu katika Halmashauri ya Msalala, MHE. Ezekiel maige ametoa pongezi kwa Serikali ya awamu ya 5 inayoongozwa na Rais Dr. John Pombe Magufuli kwa jitihada inazozifanya

za kuwaletea maendeleo watanzania ambapo amesema katika jimbo la Msalala kuna miradi mingi mikubwa ikitekelezwa, ameitaja baadhi ya miradi hiyo kuwa ni Mradi wa Maji wa ziwa Victoria kutoka

Kagongwa kwenda Isaka ambao utakamilika mwezi Novemba mwaka huu, pana mradi wa kupeleka maji katika kata za Bulyanhulu na Bugarama ambapo mkandarasi yupo eneo la kazi ombi la wananchi wa Msalala

ni kuwa Mkandarasi aongezee spidi ili mradi uanze kutumika. Pia pana upanuzi wa kituo cha Afya Chela sambamba na kupandisha hadhi zahanati za Ngaya na Isaka kuwa Vituo vya Afya ambapo utekelezaji

huu utafanyika katika mwaka huu wa fedha, haya yote yamefanyika kupitia Serikali ya awamu ya tano ikishirikiana na wadau mbalimbali.


MHE. Maige ameendelea kuiomba Serikali kutoa kipaumbele katika ujenzi wa barabara ya Kahama Geita kwani uwepo wa barabara hii utachochea maendeleo kwa watu wa Msalala na kahama kwa ujumla. Mwisho

amemwomba Waziri Mkuu awaeleze wananchi wa Halmashauri ya Msalala hatma ya ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza mabomba kwani pamekuwa na sintofahamu juu ya suala hili.


Katika salamu zake waziri mkuu MHE. Kassim Majaliwa kwa wananchi wa Msalala, MHE. Waziri mkuu amewashukuru wananchi kwa mapokezi mazuri waliyompatia na amewatoa wasiwasi kwa kusema kiwanda cha kutengeneza

mabomba ya kusafirishia mafuta ghafi kitajengwa Isaka kwa kuwa pana miundombinu yote muhimu inayohitajika na hivyo kuwataka wananchi kujenga nyumba nzuri za kulala wageni sambamba na kujenga hoteli nzuri

kwani wageni wengi watakuja kwa kuwa serikali inajenga Reli ya umeme ya Mwanza Dares salaam, Tabora Kigoma Mpanda na Isaka Rwanda ambapo Isaka ni sehemu ya katikati na ni bandari ya nchi kavu hivyo wananchi

wachangamkie fursa hii.


MHe. Waziri mkuu amewataka watumishi wa Serikali kuwatumikia wananchi kikamilifu kwani serikali ya awamu hii haitamvumilia mtumishi yeyote atakaekwenda kinyume na sheria, kanuni na taratibu za kiutumishi.

MHE. Kassim Majaliwa amewataka wananchi wa Halmashauri ya Msalala kuunga mkono jitihada za MHE. Rais za kuwezesha wananchi wanaoishi vijijini kuunganishwa na huduma ya umeme kwani Serikali imeviingiza vijiji

vyote vya Halmashauri ya Msalala katika awamu ya tatu ya utekelezaji wa mradi wa Umeme vijijini ( REA III ). Katika mradi huu MHE. Rais John Pombe magufuli ameshusha gharama za kuunganisha umeme toka Tsh. 380,000

hadi Tsh. 27000 bila kujali nguzo ngapi zitatumika.


Ziara hii itaendelea kesho katika Halmashauri ya Mji wa Kahama na Ushetu na itahitimishwa tarehe 17/07/2018 kwa kutembelea kituo cha Afya Chela na kuweka jiwe la msingi na kuzindua soko na ghala la kuhifadhi mazao

katika kata za Chela na bulige, kata zote zikiwa katika Halmashauri ya Msalala.


Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Halmashauri ya Msalala.

Matangazo

  • Bofya hapa kupata Orodha ya watakaofanya Usaili kwa ajili ya kuboresha Daftari la Wapiga Kura August 02, 2024
  • PAKUA HAPA MATOKEO YA USAILI TAREHE 10.10.2024 October 10, 2024
  • PAKUA ORODHA YA WATAKAOFANYA USAILI WA ANA KWA ANA 10-09-2023 September 09, 2023
  • Pakua Tangazo la nafasi za kazi la 08.07.2024 July 10, 2024
  • Tazama yote

Habari mpya

  • MAELEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA

    September 26, 2024
  • Mashujaa wa Michezo ya watumishi nchini wapongezwa.

    September 13, 2024
  • Mkurugenzi Mtendaji ahimiza jamii kufanya mazoezi

    September 09, 2024
  • Hamasa la vijana lafunika mbio za mwenge

    August 14, 2024
  • Tazama yote

Video

Hamasa kwa jamii kujitokeza kugombea uongozi Mamlaka ya Serikali za Mitaa
Video

Viunganishi vya Haraka

  • MKATABA WA KUKODISHA MITAMBO

Viunganishi fanano

  • TAMISEMI Website
  • Shinyanga Website
  • Ajira portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Habari, Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Anuani Nyingine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Msalala. Haki zote zimehifadhiwa.